Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 1:42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

42 akasema kwa sauti kubwa: “Wewe umebarikiwa kuliko wanawake wote, na mutoto utakayemuzaa amebarikiwa!

Gade chapit la Kopi




Luka 1:42
13 Referans Kwoze  

Wakasema: “Abarikiwe mufalme anayekuja kwa jina la Bwana! Amani mbinguni na utukufu kwa Mungu anayekuwa juu!”


“Abarikiwe kuliko wanawake wote Yaeli, muke wa Heberi Mukeni. Amebarikiwa kuliko wanawake wote wanaokaa katika mahema.


Malaika akamufikia kwenye nyumba yao na kumwambia: “Salamu kwako, wewe uliyejaliwa neema kutoka kwa Mungu! Bwana yuko pamoja nawe.”


Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.”


kwa maana ameniangalia kwa huruma, mimi mujakazi wake munyenyekevu. Tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri,


Kwa musaada wako, amepata utukufu sana; wewe umemujalia sifa na heshima.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Wao ni wazao wa babu zetu, na Kristo alizaliwa kimwili katika kizazi chao. Yeye ndiye mukubwa kupita wote na Mungu anayesifiwa kwa milele! Amina.


Moyo wangu umejaa mawazo mazuri: ninamutungia mufalme mashairi yangu, ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi hodari.


Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mutoto akajitingiza ndani ya tumbo lake. Elizabeti akajazwa na Roho Mutakatifu,


Namna gani nimepata bahati hii ya kutembelewa na mama ya Bwana wangu?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite