Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 1:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Mimba ya Elizabeti ilipotimiza miezi sita, Mungu akamutuma malaika Gabrieli katika muji mumoja wa Galilaya, unaoitwa Nazareti.

Gade chapit la Kopi




Luka 1:26
8 Referans Kwoze  

Kule akakaa katika muji ulioitwa Nazareti, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa mutu wa Nazareti.”


Malaika akamujibu: “Mimi ni Gabrieli, anayebaki karibu na Mungu! Nimetumwa kusema nawe, kwa kukuletea habari hii njema.


Wengine wakasema: “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine wakasema: “Basi Kristo angeweza kutokea Galilaya?


Basi Yosefu naye vilevile akaondoka katika muji Nazareti, wa jimbo la Galilaya, na kwenda Yudea katika muji wa kuzaliwa wa mufalme Daudi, unaoitwa Betelehemu. Alienda kule kwa sababu alikuwa mutu wa ukoo wa Daudi.


Nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka katika muto Ulayi ikiita: Gabrieli, umwelezee mutu huyu maana ya maono aliyoona.


yule mutu Gabrieli, ambaye nilikuwa nimemwona katika maono hapo mbele, alishuka kwa haraka mpaka pahali nilipokuwa. Ilikuwa wakati wa kutoa sadaka ya magaribi.


Wakati wazazi wa Yesu walipokwisha kutimiza kanuni zote zilizoagizwa na Sheria ya Bwana, wakarudia pamoja naye Galilaya, katika muji wao wa Nazareti.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite