Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 8:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Muungane, enyi watu wa mataifa, na kufezeheshwa! Musikilize, enyi inchi za mbali katika dunia! Mujiweke tayari na kufezeheshwa. Mujiweke tayari na kufezeheshwa.

Gade chapit la Kopi




Isaya 8:9
24 Referans Kwoze  

Hakika mwovu hataepuka kuazibiwa, lakini wenye haki wataokolewa.


Mufalme Ahabu wa Israeli akajibu: “Mumwambie mufalme Beni-Hadadi kwamba shujaa anajisifu kisha kupigana vita, na si mbele ya vita!”


Mutu yeyote akikuja kukushambulia, hatakuwa ametumwa nami. Yeyote atakayekushambulia, ataangamia mbele yako.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Basi Yawe atawafundisha kama watoto wadogo: kanuni juu ya kanuni, mustari juu ya mustari; mara hiki, mara hiki! Nao watalazimishwa kukimbia lakini wataanguka machalichali, watavunjika, watanaswa na kutekwa.


Musimwogope mufalme wa Babeli munayemwogopa; musimwogope hata kidogo. Mimi niko pamoja nanyi kwa kuwaokoa na kuwaponyesha kutoka katika mikono yake.


Yawe anasema hivi: Wewe Babeli ni nyundo na silaha yangu ya vita; ninakutumia kwa kuyavunjavunja mataifa, ninakutumia kwa kuangamiza falme.


Ujitayarishe, uikae wewe mwenyewe na kundi lako lote pamoja na wengine wote unaokuwa nao, uwalinde.


Wafalme hawa wote wakaungana na kupiga kambi yao katika chemichemi ya Meromu kusudi wapigane na Waisraeli.


Mutayarishe ngao ndogo na kubwa musonge mbele kwa kupigana vita.


Mutandike farasi na kupanda juu yao. Mushike nafasi zenu, na muvae kofia za chuma. Munoe mikuki yenu, muvae nguo zenu za chuma.


Kisha siku nyingi utaitwa kuishambulia inchi ambayo watu wengi waliletwa kutoka mataifa mengi na sasa wanaishi bila vitisho vya vita. Utaishambulia milima ya Israeli ambayo hapo zamani ilikuwa jangwa na matongo kwa muda murefu, lakini sasa watu wote huko wanaishi kwa usalama.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite