Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 8:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima.

Gade chapit la Kopi




Isaya 8:19
28 Referans Kwoze  

Saulo alikufa kwa sababu ya kutokuwa mwaminifu; hakukuwa mwaminifu maana hakutii neno la Yawe na alikwenda kwa mwaguzi kumwomba shauri,


Kama mutu yeyote anawaendea waaguzi wa mizimu na wachawi na hivyo kukosa uaminifu kwangu, nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake.


Na aliwatoa wana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto katika bonde la mwana wa Hinomu. Alipiga ramuli, aliaguza na alitumia hirizi; hata alishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Kisha wakajiunga kumwabudu Bali kule Peori, wakakula sadaka zilizotambikiwa kwa mizimu.


Musiwaendee waaguzi wa mizimu wala wachawi kwa kuwaomba wawaaguzie. Mukifanya hivi, mutajichafua. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Utaangushwa mbali sana ndani ya udongo, kutoka kule mbali utatoa sauti, maneno yako yatatoka kule chini katika mavumbi, sauti yako itatoka ndani ya udongo kama ya muzimu.


Nitawaondolea Wamisri uhodari wao. Nitaivuruga mipango yao. Watatafuta shauri kwa sanamu na mizimu, wachawi, mizuka na pepo.


Basi, Saulo akajigeuza na kuvaa nguo zingine, akaenda kule pamoja na watu wake wawili. Walifika kwa yule mwanamuke usiku. Saulo akamwambia: “Unifanyie uaguzi na kunipandishia mutu yeyote nitakayekutajia.”


wala muchawi, wala mulozi, wala mwenye kutaka shauri kwa mizimu na pepo au kutoka kwa wafu.


Lakini Yawe ni Mungu wa kweli, Mungu Mwenye Uzima, mufalme wa milele. Akikasirika, dunia inatetemeka, mataifa hayawezi kuvumilia hasira yake.


Naye alimutoa mwana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Alipiga ramuli; aliaguza akishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Lakini malaika wa Yawe akamwambia nabii Elia wa muji wa Tisibe, aende kukutana na wajumbe hao na kuwauliza: “Kwa nini munakwenda kwa Bali-Zebubu, mungu wa Ekuroni? Hakuna Mungu katika inchi ya Israeli?


Tena, kusudi mufalme Yosia atimize sheria zote zilizoandikwa katika kitabu Kuhani Mukubwa Hilkia alichokipata katika nyumba ya Yawe, aliondoa wachawi, watabiri, miungu, sanamu za miungu pamoja na vyombo vingine vilivyotumika kwa kuabudu miungu ya uongo kutoka inchi ya Yuda na kutoka Yerusalema.


Samweli akasema: “Kwa nini unaniomba shauri ikiwa Yawe amekuachilia na amekuwa adui yako?


Zamani manabii wa uongo walitokea kati ya watu, na ndivyo hivyo walimu wa uongo watakavyotokea kati yenu. Watu hawa wataingiza mafundisho mabaya sana ya uongo kwa siri, wakimukataa hata Bwana aliyewakomboa na kujiletea maangamizi upesi.


Yule mwanamuke akamwuliza: “Nikupandishie nani kutoka kule?” Saulo akajibu: “Unipandishie Samweli.”


Wao wenyewe wanaeleza namna mulivyotupokea wakati tulipofika kwenu na namna mulivyoacha kuabudu sanamu na kumurudilia Mungu. Mulifanya vile kusudi mumutumikie Mungu mwenye uzima na wa kweli


Siku moja tulipokuwa tukienda kule kwenye nafasi ya kufanyia maombi, tukakutana na mujakazi mumoja. Yule mwanamuke alikuwa na pepo wa kuaguza ndani yake. Na kwa njia ya uaguzi ule aliwatajirisha wabwana wake.


Yale masuke saba membamba yakameza yale masuke saba mazuri. Basi, mimi nikawaambia wachawi ndoto hizo lakini hakuna mutu aliyeweza kunifafanulia.”


Watu hao wamekufa, wala hawataishi tena; wamekuwa mizimu, wala hawatafufuka. Maana wewe umewaazibu na kuwaangamiza, hakuna atakayeweza kuwakumbuka tena.


Bila kutaka shauri langu, wanafunga safari kwenda Misri, kukimbilia ulinzi kwa mufalme wa Misri, kupata pahali pa kujificha katika inchi yake.


Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mungu, Muumba wa Israeli anasema hivi: Munataka kuniuliza juu ya watoto wangu, au kuniamuru juu ya kazi zangu mwenyewe?


Endelea basi na uganga wako, tegemea wingi wa uchawi wako. Wewe uliyashugulikia tangu ujana wako ukitumainia kwamba utafanikiwa au kusababisha woga kwa watu!


Wewe umejichokesha bure na washauri wako. Basi, wajitokeze hao wenye akili wakuokoe! Wao wanagawanya mbingu sehemusehemu, wanachunguza nyota na kutabiri kila mwezi yatakayokupata.


Basi, ninyi musiwasikilize manabii wenu, wapiga ramuli wenu, wafasiriaji wenu wa ndoto, waaguzi wenu au wachawi wenu, wanaowaambia kwamba musimutii mufalme wa Babeli.


Nitaziharibu sanamu zenu, na nguzo zenu za ibada; nanyi mutakoma kuabudu vitu mulivyotengeneza wenyewe.


Kusikuwe mutu yeyote kati yenu anayemupitisha kwenye moto mutoto wake mwanaume au mwanamuke kuwa tambiko, wala mutu anayepiga ramuli, wala mwaguzi, wala mwenye kufanya uganga,


Halafu Saulo akawaambia watumishi wake: “Munitafutie mwanamuke ambaye anaweza kuaguza kusudi nimwendee na kumwomba shauri.” Watumishi wake wakamujibu: “Kuna mwanamuke mwaguzi mumoja kule Endori.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite