Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 8:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Watu wengi watajikwaa, wataanguka na kupondekana; watanaswa katika mutego huo na kukamatwa mateka.

Gade chapit la Kopi




Isaya 8:15
12 Referans Kwoze  

Anayeanguka juu ya jiwe hili atavunjikavunjika, na yule litakayemwangukia, atapondekana.]”


Basi Yawe atawafundisha kama watoto wadogo: kanuni juu ya kanuni, mustari juu ya mustari; mara hiki, mara hiki! Nao watalazimishwa kukimbia lakini wataanguka machalichali, watavunjika, watanaswa na kutekwa.


Lakini sisi tunamuhubiri Kristo aliyetundikwa juu ya musalaba, na mahubiri hayo yanahesabiwa kama kikwazo kwa Wayuda na upumbafu kwa watu wa mataifa mengine.


Kwa sababu gani? Kwa sababu walitafuta haki ile, si kwa njia ya imani, lakini kwa njia ya matendo. Walijikwaa juu ya “lile jiwe la kukwalisha,”


Basi kwa sababu ya maneno haya, wengi kati ya wanafunzi wake wakamwacha, nao hawakutembea tena pamoja naye.


Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”


Heri mutu yule mimi sitakayekuwa kikwazo kwake!”


Kama vipofu tunapapasapapasa ukuta; tunasitasita kama watu wasiokuwa na macho. Tunajikwaa muchana kati, sawa vile ni usiku; kati ya wenye afya, sisi ni kama wafu.


nao watatoa maziwa kwa wingi hata aweze kula siagi. Watu watakaobaki katika inchi watakula maziwa na asali.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitawawekea watu hawa vikwazo, ambavyo vitawaangusha chini. Wababa na wana wataangamia, na jirani na rafiki vilevile.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite