Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 8:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mimi nitakuwa kimbilio. Nitakuwa vilevile kama jiwe la kujikwaa, jiwe kubwa la kuziangusha falme za Israeli na Yuda. Nitakuwa mutego wa kuwatega na kuwanasa wakaaji wa Yerusalema.

Gade chapit la Kopi




Isaya 8:14
24 Referans Kwoze  

Tena imeandikwa kwamba: “Jiwe lile ni la kukwalisha watu, nalo ni la kuwaangusha.” Wamejikwaa kwa sababu hawakuamini neno la Mungu, na hivi ndivyo walivyopanga kwa ajili yao tangu mwanzo.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,


Lakini, uwaambie hao wanaokuwa katika uhamisho kwamba Bwana wao Yawe anasema hivi: Ingawa nimewapeleka mbali kati ya mataifa na kuwasambaza katika inchi zingine, hata hivyo, mimi nipo pamoja nao huko wanakokuwa, kama vile hekalu kwao.


Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama.


Walinipa sumu ndani ya chakula, na nilipokuwa na kiu wakanipa divai inayochacha.


Atawanyeshea waovu makaa ya moto na kiberiti; upepo mukali utakuwa ndio azabu yao.


Na kwa hiyo akakuwa kikwazo kwao. Lakini Yesu akawaambia: “Nabii hakosewi heshima fasi zote, isipokuwa tu katika muji wake na katika jamaa yake.”


Mukuje watu wangu, muingie ndani ya nyumba zenu, mujifungie humo ndani. Mujifiche kwa muda mufupi, mpaka kasirani ya Yawe ipite.


Ni nani anayeweza kumupa Mungu kitu kwanza, kusudi naye apate kumurudishia?”


sawa mutego. Kwa maana Siku ile itawafikia watu wote wa dunia.


Utukufu wake utakuwa kwao kivuli kwa kuwakinga na joto la muchana; na kimbilio na kikingio chao wakati wa zoruba na mvua.


Anayeanguka juu ya jiwe hili atavunjikavunjika, na yule litakayemwangukia, atapondekana.]”


Ee Yawe, unilinde na makucha ya wabaya; unikinge na watesaji wakali ambao wamepanga kuniangusha.


Maana, mbele mutoto huyo hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, inchi za wafalme hao wawili unaowaogopa zitakuwa ukiwa.


Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;


Kama vipofu tunapapasapapasa ukuta; tunasitasita kama watu wasiokuwa na macho. Tunajikwaa muchana kati, sawa vile ni usiku; kati ya wenye afya, sisi ni kama wafu.


Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitawawekea watu hawa vikwazo, ambavyo vitawaangusha chini. Wababa na wana wataangamia, na jirani na rafiki vilevile.


Tena, kama mutu wa haki akigeuka katika haki yake na kutenda uovu, nami nikimwekea kikwazo, mutu huyo atakufa. Kwa vile haukumwonya, atakufa kwa sababu ya zambi yake, nayo matendo yake ya haki hayatakumbukwa. Lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.


Basi, Yoshua pamoja na jeshi lake lote na mashujaa wakaondoka Gilgali.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite