Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Yawe alinionya kwa nguvu nisifuate njia za watu hawa, akaniambia:

Gade chapit la Kopi




Isaya 8:11
10 Referans Kwoze  

Basi, Roho akaninyanyua juu na kunipeleka mbali. Yawe alinijaza uwezo wake. Nami nikaenda nikiwa na uchungu na hasira katika roho yangu.


Kwa maana sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”


Lakini ninaposema “Sitamutaja tena Yawe, wala sitasema tena kwa jina lake”, ndani yangu kunawaka kitu kama moto uliofungiwa ndani ya mifupa yangu. Ninajaribu sana kuuzuia humo, lakini ninashindwa.


Ee Yawe, wewe umenidanganya, nami kweli nimedanganyika; wewe una nguvu kuliko mimi, nawe umeshinda. Nimekuwa mutu wa kuchekelewa kila siku, kila mutu ananizarau.


Basi, Yawe akasema hivi: Kama ukinirudilia, nitakurudisha katika hali yako ya mbele, nawe utanitumikia tena. Kama ukisema maneno ya maana, yasiyokuwa ya upuuzi, basi utakuwa musemaji wangu. Watu watakufikia wewe, wala si wewe utakayehitaji kuwaendea.


Wewe mwana wangu usiandamane nao, uzuie muguu wako usifuatane nao.


Mungu anasema: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayofuata. Nitakushauria kwa uangalifu mukubwa.


Nguvu ya Yawe ikamufikia Elia, naye akajitayarisha kusafiri, akakimbia na kumutangulia Ahabu kuingia ndani ya muji Yezereheli.


Ole watoto waasi, wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu! –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite