Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mufalme wa Yuda alipopata habari kwamba Waaramu wanashirikiana na Waisraeli, yeye pamoja na watu wote wa Yuda waliogopa na kutetemeka kama miti inayotikiswa na upepo.

Gade chapit la Kopi




Isaya 7:2
28 Referans Kwoze  

Musijiunge nao katika mashauri yao mabaya, wala musiogope yale wanayoyaogopa wala kuwa na hofu.


Basi, Isaya akamujibu: Musikilize basi, enyi watu wa ukoo wa Daudi! Haitoshi kuwachokesha watu hata sasa munataka kumuchokesha Mungu wangu vilevile?


Kuta za matofali zimeanguka lakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa! Nyumba za nguzo za mikuyu zimeharibiwa lakini pahali pake tutajenga za mierezi.


Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.


Mufalme Herode aliposikia maneno haya, akafazaika sana pamoja na wakaaji wote wa Yerusalema.


Watu wa Efuraimu wananizunguka kwa uongo, na Waisraeli kwa udanganyifu. Lakini watu wa Yuda wanaendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu Mutakatifu.


Enyi jamaa ya Daudi, Yawe anasema hivi: Kila asubui muamue maneno kufuatana na sheria yangu, muwakomboe wote walionyanganywa mali zao toka katika mikono ya watesaji. Kama si vile, hasira yangu itawaka kama moto, wala hakuna atakayeweza kuizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Wakaaji wake wakiwa wameishiwa nguvu, wametishika na kufazaika, wamekuwa kama mimea ya shamba, kama majani changa, kama majani yanayoota juu ya paa, yanayokauka mbele ya kukomaa.


Nitaweka juu ya bega lake ufunguo wa ukoo wa Daudi. Akifungua, hakuna atakayeweza kufunga na akifunga, hakuna atakayeweza kufungua.


Wivu wa Efuraimu juu ya Yuda utakoma, hakutakuwa tena uadui kati ya Yuda na Efuraimu.


Yawe atakuletea wewe pamoja na watu wako na jamaa yote ya kifalme siku za taabu kuliko zile zote zilizotokea tangu wakati watu wa Efuraimu walipojitenga na watu wa Yuda; ni kusema, atawaletea ninyi mufalme wa Asuria.


Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Yawe ni kimbilio langu; namna gani basi munaweza kuniambia: “Ruka kama ndege, mpaka kwenye milima,


Nao wakubwa fulani wa Efuraimu, Azaria mwana wa Yohana, Berekia mwana wa Mesilemoti, Yehizikia mwana wa Salumu na Amasa mwana wa Hadilai, vilevile waliwagombeza wale waliotoka kwa vita.


Kwa hiyo Amazia akawaacha waaskari waliotoka Efuraimu warudi kwao. Basi wakarudi kwao wakiwa wamewakasirikia sana watu wa Yuda.


Mutu huyo akailaani ile mazabahu akisema: “Ee mazabahu, Yawe anasema hivi: ‘Kutazaliwa mutoto katika ukoo wa Daudi, jina lake Yosia. Huyo atawatwaa makuhani wanaotumika kwa nafasi ya ibada na kufukiza ubani juu yako, na kuwatambika juu yako. Hakika, mifupa ya watu itateketezwa juu yako!’ ”


Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mufalme hakuwajali, walimwambia: “Hatuna ushirika wowote na Daudi! Hatuna sehemu yetu kutoka kwa huyo mwana wa Yese. Murudie kwenu, enyi watu wa Israeli! Uitunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.” Hivyo, watu wa Israeli wakarudi kila mutu kwake.


Lakini yeye, nitamwachia kabila moja kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi, na kwa ajili ya Yerusalema ambao nimeuchagua kuwa wangu katika makabila yote ya Israeli.


Ukoo wako na ufalme wako vitadumu imara siku zote. Kiti chako cha kifalme kitakuwa imara milele.”


Waaramu na vilevile Peka pamoja na jeshi lake la Efuraimu wamefanya mupango mubaya juu yako. Wamesema:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite