Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 66:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.

Gade chapit la Kopi




Isaya 66:2
35 Referans Kwoze  

Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Watu wa haki wakimulilia Yawe, yeye anawasikia, na kuwaokoa katika taabu zao zote.


Ee Bwana, uniwezeshe kusema, midomo yangu itangaze sifa zako.


Basi wapendwa wangu, mulionyesha utii wenu siku zote wakati nilipokuwa kwenu, na sasa ingekuwa vema muendelee kufanya vile katika siku hizi ninapokuwa mbali nanyi. Mutumike kwa ajili ya wokovu wenu kwa woga na kutetemeka,


Heri mutu anayemwogopa Yawe siku zote, lakini mwenye moyo mugumu atapata hasara.


Ee Yawe, ingawa wewe uko juu ya wote, unawaangalia wanyenyekevu kwa wema; lakini, unatambua wenye kiburi kwa mbali.


Ninatetemeka kwa kukuogopa wewe; nimejaa hofu kwa sababu ya maamuzi yako.


Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Kwa hiyo, tufanye agano na Mungu wetu, tuachane na wanawake hawa pamoja na watoto wao, kwa kufuatana na shauri lako na la wengine wanaotii amri za Mungu. Yote yatendeke kwa kufuatana na Sheria.


Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.


Wakubwa wananitesa bila sababu, lakini mimi ninaheshimu maneno yako kwa moyo wote.


Halafu watu wote walioshikwa na hofu kwa sababu ya maneno Mungu wa Israeli aliyosema juu ya makosa ya wale waliorudi kutoka katika uhamisho wakaanza kukusanyika karibu nami nikiwa mwenye kufazaika mpaka magaribi, wakati wa kutoa sadaka.


Muinue macho yenu juu mbinguni! Ni nani aliyeziumba nyota hizo? Ni yule anayeziongoza kama jeshi lake, anayeijua hesabu yake yote, anayeziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi, hakuna hata moja inayokosekana.


Kristo alikuwa yuko mbele vitu vyote havijakuwa, na kwa njia ya kuungana naye vyote vinashikamana.


Lakini simama, uingie katika muji, na mule watakuambia jambo unalopaswa kufanya.”


Lakini sasa ninawaambia kama hapa kuna mukubwa kupita hekalu!


Ni mimi peke yangu niliyeumba vitu hivi vyote!’


Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima.


Watanifuata mimi Yawe ninayenguruma kama simba; nitakaponguruma watanifikia toka magaribi wakitetemeka.


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


“Umeona jinsi Ahabu alivyojinyenyekeza mbele yangu? Basi, kwa sababu amejinyenyekeza, sitaleta yale maangamizi atakapokuwa angali anaishi, lakini nyakati za utawala wa mwana wake nitaiangamiza jamaa ya Ahabu.”


Kisha Safanu, mwandishi akamwambia mufalme: “Kuhani Hilkia amenipa kitabu.” Naye Safanu akakisoma mbele ya mufalme.


Mufalme aliposikia maneno ya Kitabu cha Sheria, akapasua nguo zake.


Sadaka ninayokutolea, ee Mungu, ni roho munyenyekevu. Haukatai moyo munyenyekevu na wa kutubu.


Watu wataona jambo hilo, nao watatambua na kuelewa kwamba mimi Yawe nimetenda hayo, mimi Mutakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite