Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 64:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Usitukasirikie sana, ee Yawe, usiukumbuke uovu wetu siku zote! Ukumbuke kwamba sisi wote ni watu wako!

Gade chapit la Kopi




Isaya 64:8
33 Referans Kwoze  

Kwa maana sisi ni viumbe vya Mungu, na kwa kuungana kwetu na Yesu Kristo, alituumba kusudi tuishi maisha ya matendo mema, ambayo Mungu alitutayarishia tangu mbele tupate kuyatenda.


Kwa mikono yako wewe mwenyewe uliniumba; unijalie akili nijifunze amri zako.


Ee Yawe, utatimiza yote uliyoniahidia. Wema wako, ee Yawe, unadumu milele. Usisahau kazi ya mukono wako mwenyewe.


Mujue kwamba Yawe ndiye Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, sisi ni mali yake; sisi ni watu wake na kondoo wake anaowachunga.


Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.


Ninyi munafanya mambo kinyume kabisa! Mufinyanzi na udongo ni hali moja? Chombo hakiwezi kumwambia aliyekitengeneza hivi: Wewe haukunitengeneza. Kilichofinyangwa hakiwezi kumwambia aliyekiumba; Wewe haujui kitu.


Ole kwake mutu anayebishana na Muumba wake: chombo cha udongo kubishana na mufinyanzi wake! Udongo unamwuliza anayeufinyanga: Unatengeneza nini hapa? au kumwambia: Kazi yako si kamili!


Yawe, Mukombozi wako, aliyekuumba tangu katika tumbo, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe niliyeumba vitu vyote. Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu, niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!


Kila mumoja anajulikana kwa jina langu; niliwaumba wote na kuwafanya kwa ajili ya utukufu wangu.”


Yawe anasema hivi: Ewe Israeli, watu wa Yakobo, kumbuka kwamba wewe ni mutumishi wangu. Nilikuumba kusudi ukuwe mutumishi wangu, nami sitakusahau hata kidogo.


Munaweza namna gani kumulipa hivyo Yawe, enyi watu wapumbafu na wasiokuwa na akili? Yeye siye baba yenu aliyewaumba, aliyewafanya na kuwaimarisha?


Kwa maana ninyi wote mumekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani na kuungana na Yesu Kristo.


Kama ninyi ni watu wa Kristo, basi, ninyi ni wazao wa Abrahamu, ninyi mutakuwa warizi sawa vile Mungu alivyoahidi.


Nawe utamwambia mufalme wa Misri kwamba Yawe anasema hivi: ‘Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.


Ninyi munafanya matendo yale baba yenu anayofanya.” Wakamujibu: “Sisi si watoto wa haramu. Tuko na baba mumoja, naye ndiye Mungu.”


Ni sawa kwako kunionea, kuzarau kazi ya mikono yako na kupendelea mipango ya waovu?


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Yawe wa majeshi atawabariki na kusema: Wabarikiwe Wamisri watu wangu, vilevile na Waasuria ambao ni kitambulisho cha kazi yangu na Waisraeli wanaokuwa urizi wangu.


Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mungu, Muumba wa Israeli anasema hivi: Munataka kuniuliza juu ya watoto wangu, au kuniamuru juu ya kazi zangu mwenyewe?


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.


Sisi wote si watoto wa baba mumoja? Sisi wote hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Mbona basi, hatuaminiani sisi kwa sisi, na tunalizarau agano Yawe alilofanya na babu zetu?


Ukifanya hivyo, hakika Wamisri watasema: Aliwatoa kwa nia mbaya kwa kuwaua kwenye mulima na kuwateketeza kabisa katika dunia. Ee Yawe, tuliza hasira yako kali na kuacha jambo hilo baya ulilokusudia kufanya juu ya watu wako.


Maana, hawa ni watu na urizi wako, watu ambao uliwatoa kwa nguvu na uwezo wako mukubwa.


Mashairi ya Asafu. Kwa nini, ee Mungu, umetutupilia kabisa? Mbona hasira yako inawaka juu ya kondoo wako?


Mukuje tuiname chini na kumwabudu; tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu!


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Maana sitaendelea kugombana wala kuwakasirikia siku zote, maana hao niliowaumba watazimia mbele yangu, nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uzima.


Maana alisema juu yao: Hakika, hawa ni watu wangu; watoto wangu ambao hawatanidanganya. Basi yeye akakuwa Mwokozi wao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite