Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 64:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Sisi wote tumekuwa kama watu wachafu; matendo yetu yote mema ni kama nguo chafu. Wote tunanyauka kama majani, uovu wetu unatupeperusha kama upepo.

Gade chapit la Kopi




Isaya 64:5
27 Referans Kwoze  

Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


lakini katika kila taifa mutu yeyote anayemutii Mungu na kutenda yanayokuwa ya haki, anamupendeza.


Yawe wa majeshi alisema hivi: Mimi Yawe sibadiliki. Ni kwa sababu hii, ee ninyi wazao wa Yakobo, hamujateketezwa.


Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.


Lakini wao waliasi, wakaihuzunisha roho yake takatifu. Basi, Mungu akageuka, akakuwa adui yao; yeye mwenyewe akapigana nao.


Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.


Lakini wema wa Yawe unadumu milele, kwa wale wote wanaomwabudu; na haki yake inadumu vizazi vyote,


Uitafute furaha yako kwa Yawe, naye atakujalia unayotamani katika moyo.


Njia zote za Yawe ni njema na za uaminifu kwa wale wanaoshika agano lake na maagizo yake.


Mazabahu hiyo iwekwe mbele ya pazia kando ya Sanduku la Agano, mbele ya kiti cha rehema ambapo nitakutana nawe.


Mimi nitakutana nawe pale. Kutoka juu ya kiti kile cha rehema katikati ya makerubi wale wanaokuwa juu ya Sanduku la Agano, nitazungumuza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.


Ninyi mutanijengea mazabahu ya udongo. Juu yake mutanitolea kondoo wenu na ngombe wenu kama sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Pahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, pale pale mimi mwenyewe nitawafikia na kuwabariki.


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Ee Yawe, Mungu wetu, tulipata kutawaliwa na wabwana wengine ambao si wewe, lakini tunakubali wewe pekee kuwa Mungu wetu.


Nitakumbusha mema ya Yawe, sifa za Yawe, matendo yake yote kwetu, mambo mazuri aliyowatendea Waisraeli, rehema yake, na wingi wa wema wake.


Tumetenda zambi, tumekosa, tumetenda maovu na kukuasi. Tumevunja amri zako na maagizo yako.


Mutakuwa kama mialo ambayo majani yake yamekauka; kama shamba lisilokuwa na maji.


Aliwaazibu watu wake kwa kuwapeleka katika uhamisho. Wakati wa upepo mukali wa mashariki, aliwaondoa kwa pigo kali.


Kuhani Mukubwa Yoshua alikuwa akisimama mbele ya malaika, akiwa amevaa nguo zenye kuchafuka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite