Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 61:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.

Gade chapit la Kopi




Isaya 61:8
34 Referans Kwoze  

Yawe ni wa haki na anapenda watu watende kwa haki. Watu wa usawa wataona uso wake.


Siku zinakuja ambapo nitawaazibu wote waliotahiriwa kimwili tu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ni kusema nitawaazibu:


Nitafanya nao agano la milele, kwamba sitaacha kuwatendea mema hata kidogo; nitaweka ndani ya mioyo yao utii kwa ajili yangu kusudi wasiniache tena.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


maana Yawe anapenda haki, wala hawaachi waaminifu wake. Anawalinda hata milele; lakini wazao wa waovu wataangamizwa.


“Nitasimamisha agano langu nawe, wazao wako na vizazi vyao vyote milele; nitakuwa Mungu wako na Mungu wa wazao wako milele.


Ninatembea katika njia ya haki; ninafuata sheria ya Mungu.


Ee mufalme mukubwa, mupenda haki, umesimamisha usawa katika Israeli; umeleta sheria na haki.


Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako.


Kiti chako cha kifalme ni imara, kinadumu milele kama cha Mungu. Wewe unatawala watu wako kwa haki.


Yawe anapenda haki na sheria. Dunia imejaa wema wake.


Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.


Bwana aongoze mafikiri yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.


Lakini Yawe wa majeshi anatukuzwa wakati sheria yake inafuatwa. Utakatifu wa Mungu Mutakatifu unaonyeshwa wakati haki inatendwa.


Yeye anasema: “Munikusanyie waaminifu wangu, waliofanya agano nami kwa njia ya sadaka!”


Mungu anasema: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayofuata. Nitakushauria kwa uangalifu mukubwa.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


Wanadamu wote ni kama pumzi tu; wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu. Wakipimwa wote pamoja, pumzi ni nzito kuliko wao.


Alimusimamishia Yakobo ahadi yake, akamuhakikishia agano hilo la milele.


Nitatumia sheria kama kipimo changu, nitatumia haki kama timazi. Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo munaoutegemea, na mafuriko yataharibu kikingio chenu.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Milima inaweza kutoweka, vilima vinaweza kuondolewa, lakini rehema zangu kwako sitaziacha, agano langu la amani litaimarishwa. Ni Yawe anayekuhurumia anayesema hivyo.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki, maana ninakaribia kuwaokoa, watu wataona wazi kwamba ninawakomboa.


Kama vile mbingu mupya na dunia mupya nitakazoumba zitakavyodumu milele kwa uwezo wangu, ndivyo wazao wako na jina lako litakavyodumu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Munasema: Mambo haya yametuchokesha sana na munanizarau. Munaniletea sadaka za nyama muliopata kwa njia ya kunyanganya, au wanaokua vilema au wagonjwa. Basi, nipokee sadaka hizo toka katika mikono yenu?


Lakini mimi nitalikumbuka agano langu nililoagana nawe katika siku za ujana wako. Nitafanya nawe agano la milele.


Nitafanya nao agano la amani. Nitaondoa nyama wakali katika inchi, kusudi kondoo wangu wakae katika mbuga kwa usalama na kulala katika pori.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite