Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 60:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mataifa watatembea katika mwangaza wako, wafalme watavutwa na kungaa kwako.

Gade chapit la Kopi




Isaya 60:3
43 Referans Kwoze  

Kwa maana Bwana ametuagiza hivi: ‘Nimekuweka kuwa mwangaza wa mataifa, kusudi watu wapate kuokolewa katika dunia yote.’ ”


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Kwa hiyo watu wa mataifa watatembea katika mwangaza wake na wafalme wa dunia wataleta utajiri wao ndani yake.


Lakini mimi, nitakaponyanyuliwa toka katika dunia, nitawavuta watu wote kuja kwangu.”


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


kusudi watu wote wengine wamugeukie Bwana, watu wa mataifa yote wapate kuwa watu wangu wa pekee.


Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!


Watu wangu watarudia kutoka mbali, wengine kutoka kaskazini na magaribi, wengine kutoka upande wa kusini.


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Wafalme wote katika dunia watakusifu, ee Yawe, kwa sababu wameyasikia maneno yako.


Onyesha, ee Mungu, nguvu yako kubwa; nguvu yako uliyotumia kwa ajili yetu.


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Iliandikwa vilevile kwamba kwa jina lake watahubiri mataifa yote, kuanzia Yerusalema, kusudi wageuke toka katika zambi na wapate kusamehewa.


Basi muwaendee watu wa mataifa yote kusudi wapate kuwa wanafunzi wangu, mukiwabatiza kwa jina la Baba, la Mwana na la Roho Mutakatifu.


Nao Waisraeli watarizi mabaki ya inchi ya Edomu na mataifa yote yaliyokuwa yangu. –Ni ujumbe wa Yawe, yule anayefanya hivyo.


Maana Yawe anasema hivi: Nitakuletea fanaka nyingi kama muto, utajiri wa mataifa kama muto uliofurika. Nanyi mutanyonya na kubebwa kama mutoto muchanga, mutabembelezwa kama mutoto juu ya magoti ya mama yake.


Utaletewa chakula na watu wa mataifa; wafalme watakupatia chakula bora. Hapo utatambua kwamba mimi Yawe ni Mwokozi wako; mimi Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mukombozi wako.


Yawe anasema: Wageni watazijenga upya kuta zako, wafalme wao watakutumikia. Maana kwa hasira yangu nilikupiga, lakini kwa wema wangu nimekuhurumia.


Wafalme wote wa dunia wamuheshimu, watu wa mataifa yote wamutumikie.


Wamasikini watakula na kushiba; wanaomutafuta Yawe watamusifu. Mungu awajalie waishi milele!


Sasa, enyi wafalme, mutumie akili; musikilize onyo hili, enyi watawala wa dunia.


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Watu watatangaza jina la Yawe kule Sayuni; sifa zake zitatangazwa kule Yerusalema,


Mimi Yawe nimekuita kutenda haki, nimekushika mukono na kukulinda. Kwa njia yako nitafanya ahadi na watu wote, wewe utakuwa mwangaza wa mataifa.


Munigeukie mimi mupate kuokolewa, popote munapokuwa katika dunia. Maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine.


–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, yule anayewakusanya Waisraeli waliosambazwa.– Zaidi ya hao niliokwisha kukusanya, nitawakusanya watu wengine wakutane nao.


Mataifa watauona wokovu wako, wafalme wote watauona utukufu wako. Nawe utaitwa kwa jina jipya ambalo litapangwa na Yawe mwenyewe.


Mataifa yataheshimu jina la Yawe; wafalme wote katika dunia wataogopa utukufu wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite