Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 6:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kisha nikamusikia Yawe akisema: Nimutume nani? Ni nani atakayekuwa mujumbe wetu? Nami nikajibu: Niko hapa! Unitume mimi.

Gade chapit la Kopi




Isaya 6:8
23 Referans Kwoze  

Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Halafu Bwana akaniambia: ‘Kwenda, kwa maana nitakutuma mbali kwa watu wa mataifa mengine.’ ”


Yawe anasema; Nilikuwa tayari kujionyesha kwao wasiouliza habari zangu. Nilikuwa tayari kuwapokea wale wasionitafuta. Nililiambia taifa ambalo halikuomba kwa jina langu: Niko hapa! Niko hapa!


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Kisha Mungu akasema: “Tumufanye mutu kwa mufano wetu, anayefanana nasi, atawale samaki wa bahari, ndege wa anga, nyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vinavyotambaa.”


Basi, tushuke chini na kuvuruga luga yao kusudi wasielewane wao kwa wao.”


Vilipokuwa vinakwenda, nilisikia sauti ya mabawa yao; sauti ya muvumo huo ilikuwa kama ile ya maji mengi, kama sauti ya ngurumo kutoka kwa Mungu wa majeshi, na kama kelele ya jeshi. Viliposimama, vilikunja mabawa yao.


Halafu Yawe akauliza: ‘Ni nani atakayemushawishi Ahabu aende aangamie kule Ramoti-Gileadi?’ Kila mumoja akajibu namna alivyofikiri.


Shindo la mabawa ya makerubi iliweza kusikilika hata kwenye kiwanja cha inje, kama sauti ya Yawe wa majeshi anaposema.


Kisha Yawe Mungu akasema: “Sasa, mwanadamu amekuwa kama mumoja wetu, anajua mazuri na mabaya. Inafaa kumuzuia kula lile tunda la muti wa uzima, maana akilikula ataishi milele.”


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


“Kwa sababu hii, Ee mufalme Agripa, mimi nikafanya sawa nilivyoagizwa katika maono yale yaliyotoka mbinguni.


Halafu Yawe akamwita Samweli, naye Samweli, akaitika: “Niko hapa!”


Kisha nikamusikia Yawe akisema kwa sauti kubwa: Mujongee karibu ninyi mutakaouazibu muji huu. Mukuje na silaha zenu za kuangamiza.


Nyuma ya mambo yale, Mungu alimupima Abrahamu. Mungu alimwita: “Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa.”


Lakini malaika wa Yawe akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu! Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa!”


Saulo alipoangalia nyuma, aliniona, akaniita. Nilipoitika,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite