Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 6:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.

Gade chapit la Kopi




Isaya 6:13
25 Referans Kwoze  

Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.”


Wayuda wanaoa wanawake wa kigeni na kuwaoea wana wao vilevile. Hivyo, taifa takatifu la Mungu limechanganyika na watu wa mataifa mengine. Vilevile wasimamizi na wakubwa ndio wa kwanza kutenda maovu hayo.”


Na kama Bwana asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja ambaye angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya wachaguliwa aliowachagua amezipunguza.


Mungu hakuwafanya ninyi wote wawili mukuwe mwili mumoja na roho moja? Alikusudia nini alipofanya hayo? Tuzae watoto wanaomupendeza Mungu. Kwa hiyo, muchunge uzima wenu na kuhakikisha kwamba hakuna hata mumoja wenu anayekosa uaminifu kwa muke wake.


Yawe wa majeshi asingetuachia watu wachache, tungekwisha kuwa kama watu wa Sodoma tungekuwa na hali ileile ya Gomora.


Wao ni wazao wa babu zetu, na Kristo alizaliwa kimwili katika kizazi chao. Yeye ndiye mukubwa kupita wote na Mungu anayesifiwa kwa milele! Amina.


Wale watakaobaki wazima katika Yerusalema, huko Sayuni, wataitwa Wachaguliwa wa Mungu; hao ndio wale wote watakaokuwa wameandikwa katika kitabu chake waishi huko Yerusalema.


Na kama Mungu asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya watu wake aliowachagua, yeye atazipunguza.


Mufanye hivyo kwa sababu ninyi mumetakaswa kwa Yawe, Mungu wenu. Kati ya watu wote katika ulimwengu aliwachagua ninyi kusudi mukuwe taifa lake mwenyewe.


Kutatokea chipukizi katika shina la Yese, tawi litachipuka toka mizizi yake.


Hata hivyo, nitawaacha wengine wabaki wazima; wamoja kati yenu wataponyoka upanga nao watasambazwa katika inchi mbalimbali.


Maana Bwana wetu Yawe anasema: Itakuwa hivi: juu yenu ninyi Waisraeli: Watu elfu moja wanatoka katika muji kwenda kupigana lakini watarudia watu mia moja tu; wataondoka watu mia moja wa kijiji kimoja lakini watu kumi tu wataponyoka.


Sehemu mbili za tatu za watu katika inchi zitaangamizwa; ni sehemu moja ya tatu tu itakayobaki.


Ijapokuwa ninyi ni wengi kama nyota za mbinguni, lakini mutakuwa wachache tu kwa sababu hamukutii sauti ya Yawe, Mungu wenu.


Lakini sasa, ee Yawe, Mungu wetu, kwa muda mufupi umetuonyesha huruma yako na kuwawezesha wamoja kati yetu kuponyoka kutoka katika utumwa na kuishi kwa usalama pahali pako patakatifu. Pahali pa utumwa, umetupa furaha na maisha mapya.


Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima wataenea kati ya mataifa mengi, watakuwa kama umande unaotoka kwa Yawe, kama manyunyu yanayoanguka kwenye majani ambayo hayasababishwi na mutu wala kumutegemea mwanadamu.


Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevu ambao watakimbilia usalama kwangu mimi Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite