Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 6:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Nami Yawe nitawapeleka watu mbali, na kuifanya inchi yote kuwa matongo.

Gade chapit la Kopi




Isaya 6:12
15 Referans Kwoze  

Kelele la waaskari wapanda-farasi na la wapiga mishale litakaposikilika, watu wote watakimbia. Wamoja wao watakimbilia katika vichaka, wengine watajificha katikati ya mawe. Kila muji utaachwa tupu; hakuna mutu atakayekaa ndani yake.


Yawe atawatawanya kati ya mataifa yote, kutoka pembe moja ya dunia mpaka nyingine na huko mutaitumikia miungu mingine ya miti na mawe, miungu ambayo ninyi wala wazee wenu hamukuijua.


Sababu gani umetusahau kwa muda murefu hivyo na kutuacha siku nyingi hivyo?


Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha kwa falme zote za dunia, kwa sababu ya mambo ambayo Manase mwana wa Hezekia, aliyofanya kule Yerusalema, alipokuwa mufalme wa Yuda. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe anasema hivi: Nimeiacha nyumba yangu; nimeitupa mali yangu mimi mwenyewe. Israeli, mupenzi wangu wa moyo, nimemutoa katika mikono ya waadui zake.


Umezidisha taifa letu, ee Yawe, umelizidisha taifa letu. Umeipanua mipaka yote ya inchi, kwa hiyo wewe unatukuzwa.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli akawapiga na kuwaua watu hao kule Ribla katika inchi ya Hamati. Hivyo watu wa Yuda wakapelekwa kuwa watumwa inje ya inchi yao.


Nebuzaradani, mukubwa wa waaskari wa mufalme, akawapeleka katika uhamisho watu waliokuwa wamebakia katika muji na wale wote waliokuwa wamejitoa wenyewe kwa mufalme wa Babeli pamoja na watu wengine wote.


Kwa maana ikiwa kukataliwa kwao na Mungu kumeleta upatanisho kati yake na dunia, basi si hakika kwamba kukubaliwa kwao na Mungu kutaleta uzima kwa wale waliokufa.


Nimemusikia Yawe wa majeshi akisema hivi: Hakika nyumba nyingi zitabaki tupu, zile kubwa na nzuri zitabaki wazi bila wakaaji.


Nitawafanya watu kuwa wachache kuliko zahabu safi; wanadamu watakuwa wachache kuliko zahabu ya Ofiri.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli aliwapiga na kuwaua watu hao kule Ribla katika inchi ya Hamati. Basi, hivi ndivyo watu wa Yuda walikwenda katika uhamisho inje ya inchi yao.


wanadamu, nyama, ndege na samaki. Vyote nitaviangamiza. Waovu nitawaangamiza kabisa; wanadamu nitawateketeza kabisa katika dunia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite