Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 6:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika mwaka mufalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana katika maono akiikaa katika kiti cha kifalme kinachoinuka juu sana. Pindo la nguo yake lilienea katika hekalu lote,

Gade chapit la Kopi




Isaya 6:1
38 Referans Kwoze  

Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliona kwa mbali utukufu wa Yesu, naye alisema habari zake.


Hekalu likajaa moshi kutokana na utukufu wa Mungu na uwezo wake. Na hakuna mutu aliyeweza kuingia ndani ya hekalu mpaka yale mapigo yaliyoletwa na wale wamalaika saba yalipotimizwa.


Nilipokuwa nikiendelea kuangalia, nikaona viti vya kifalme viliwekwa hapo, kisha Muzee mumoja wa zamani sana akakuja, akaikaa. Alikuwa amevaa nguo nyeupe kama teluji; nywele zake zilikuwa kama sufu safi. Kiti chake cha kifalme kilikuwa ndimi za moto, na magurudumu ya kiti kile yalikuwa moto unaowaka.


Nani anayekuwa kama Yawe, Mungu wetu? Yeye anakaa juu kabisa;


“Wakati Mwana wa Mutu atakapokuja katika utukufu wake pamoja na wamalaika wote, ataikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu.


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


Yawe anasema hivi: Mbingu ni kiti changu cha kifalme, dunia ni kiti cha kupumzikishia miguu yangu. Mutanijengea nyumba ya namna gani basi, pahali nitakapoweza kupumzikia?


Wema wako ni mukubwa kuliko mbingu; uaminifu wako unaenea hata kwenye mawingu.


Na mara moja nikashikwa na Roho wa Mungu. Nikaona kiti cha kifalme kimewekwa kule mbinguni na mutu mumoja alikuwa akiikaa juu ya kiti kile.


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


Anakomesha vita popote katika dunia. Anavunjavunja pinde na mikuki, nayo magari ya vita anayateketeza.


Kisha nikaona kizingo cha karatasi katika mukono wa kuume wa yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme. Kizingo kile kilikuwa kimeandikwa ngambo na ngambo na kufungwa kwa vifundo saba vya mihuri.


Ni yeye tu asiyeweza kufa na anayekaa katika mwangaza ambao mutu hawezi kukaribia. Hakuna mutu aliyemwona wala hakuna mutu anayeweza kumwona. Ndiye mwenye heshima na uwezo wa milele! Amina.


Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.


Mimi ninaongea naye kinywa kwa kinywa, waziwazi na si kwa kutumia mafumbo. Yeye ameliona umbo langu mimi Yawe. Kwa nini, basi, hamukuogopa kusema vibaya juu ya mutumishi wangu Musa?


wale wazee makumi mbili na wane waliinama uso mpaka chini mbele ya yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakimwabudu huyo anayeishi kwa milele na milele. Nao walikuwa wakikuja kuweka taji zao mbele ya kiti chake, na kusema:


Kisha nikaona kwamba katika lile anga juu ya vichwa vya makerubi kulikuwa kitu kinachofanana na jiwe la rangi ya samawi, umbo lake kama kiti cha kifalme.


Kwa siku ya tano ya mwezi wa ine, mwaka wa makumi tatu, wakati nilipokuwa katikati ya wale watu waliopelekwa katika uhamisho, karibu na muto Kebari, mbingu zikafunguka, nikapata maono toka kwa Mungu.


Siku hiyo mutasema: Mumushukuru Yawe, muombe kwa jina lake. Mujulishe kwa mataifa matendo yake, mutangaze kuwa jina lake limetukuzwa.


Nao wakaiambia milima na mawe: “Mutuangukie na kutufunika mbali na yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme na mbali na kasirani ya Mwana-Kondoo.


Azaria akakufa na kuzikwa katika makaburi ya wafalme katika muji wa Daudi; na mwana wake Yotamu akatawala kwa pahali pake.


Yule Mwana-Kondoo akajongea na kukamata kizingo kutoka mukono wa kuume wa yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme.


Mutu yule aliangaa kama mawe ya bei kali ya yaspi na sardio. Kiti kile cha kifalme kilikuwa kimezungukwa na upindi wa mvua uliongaa kama jiwe la zumaridi.


Vile viumbe vine vya ajabu viliimba kwa kumutukuza, kumuheshimia na kumushukuru yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme, yule anayeishi kwa milele na milele. Kila mara vilipofanya vile,


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


Kisha Mikaya akasema: “Basi sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akikaa katika kiti chake cha kifalme na jeshi lake lote la mbinguni likisimama upande wake wa kuume na wa kushoto.


Utukufu wa Yawe ukapanda juu tokea wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha nyumba hiyo, na lile wingu likaijaza nyumba, na kiwanja kilijaa mwangaza wa utukufu wa Yawe.


Mimi ni kama mutumwa mbele ya bwana wake. Ninaweza namna gani kusema nawe? Sina nguvu na pumzi imeniishia!


Kisha Musa, Haruni, Nadabu na Abihu na wazee makumi saba wa Israeli wakapanda juu ya mulima,


Kweli nilikuwa nimesikia habari zako kwa masikio tu, lakini sasa ninakuona kwa macho yangu mwenyewe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite