Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 59:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Wavu wenu haufai kama nguo, watu hawawezi kujifunikia munachofuma. Kazi zenu ni kazi za uovu, matendo yenu yote ni mateso makali.

Gade chapit la Kopi




Isaya 59:6
31 Referans Kwoze  

Kama vile maji yanavyotiririka toka ndani ya kisima, ndivyo maovu yanavyotiririka katika Yerusalema. Mateso makali na maangamizi yanasikilika ndani yake. Ninaona magonjwa na vidonda mbele yangu kila siku.


Munafikiri kwamba munafanya sawa, lakini nitayafichua matendo yenu, nayo miungu yenu haitawafalia kitu.


Siku hiyo nitawaazibu wote wanaoruka kizingiti cha nyumba kama wapagani, wanaojaza nyumba ya bwana wao vitu vya mateso na udanganyifu.


Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.


Lakini Yawe anawaambia ninyi hivi: Munawatendea watu wangu kama adui. Munawanyanganya watu watulivu nguo zao; watu wanaopita kwenda zao bila wasiwasi, na wasiokuwa na mafikiri yoyote ya vita.


Ninyi munajaribu kuifukuza ile siku mbaya. Lakini munaukaribisha utawala wa mateso.


Hawajui kabisa kutenda mambo yanayokuwa sawa! –Ni ujumbe wa Yawe.– Wamejaza nyumba zao nzuri na vitu vya wizi na mateso.


Tengeneza munyororo; kwa maana inchi imejaa makosa ya umwangaji wa damu na muji umejaa mateso makali.


Mateso makali yanaendelea kuwa mubaya zaidi. Hakuna hata mumoja kati yenu atakayebaki, wala vitu mulivyojilundikia kwa wingi au utajiri wenu; hakutakuwa mutu mwenye heshima kati yenu.


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Munafunga kula lakini munagombana na kupigana mangumi vikali. Mukifunga namna hiyo, maombi yenu hayatafika kwangu juu.


Ole watoto waasi, wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu! –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Enyi watawala, munasema kwa haki kweli? Munawahukumu watu kwa usawa?


Mungu aliona kwamba dunia imeharibika na kujaa mateso makali.


ingawa sijatesa watu kwa mukono wangu, na maombi yangu kwa Mungu ni safi.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ninachukia kuachana. Ninachukia wakati mumoja wenu anapomutendea muke wake ubaya ule. Muhakikishe kwamba hakuna hata mumoja wenu anayekosa uaminifu kwa muke wake.


vikiuzunguka muchana na usiku, na kuujaza hasara na ukorofi.


Naye akaniambia: Uovu wa Waisraeli na watu wa Yuda ni mukubwa sana. Inchi imejaa umwagaji wa damu na katika muji hakuna haki, kwa maana wanasema: Yawe ameiachilia inchi; Yawe haoni.


Ole wake Yerusalema, muji wa uasi, muchafu, na wenye kujaa watesaji.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite