Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 59:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Makosa yetu mbele yako ni mengi sana, zambi zetu zinashuhudia juu yetu. Kweli, makosa yetu yanaandamana nasi, tunayajua maovu yetu.

Gade chapit la Kopi




Isaya 59:12
31 Referans Kwoze  

nikisema: “Ee Mungu wangu, ninaona haya kubwa sana kukiinua kichwa changu mbele yako. Zambi zetu zimelundikana kupita hata vichwa vyetu; makosa yetu yanafika hata mbinguni.


Kiburi cha Waisraeli kinaonekana wazi; watu wa Efuraimu watajikwaa katika makosa yao, nao watu wa Yuda watajikwaa pamoja nao.


Kuapa, uongo, mauaji, wizi na uzinzi vinatokea humo. Umwangaji wa damu unafuatana kwa mufululizo.


Lakini wakaaji wake wameyaasi maagizo na masharti yangu, wakakuwa wabaya kuliko mataifa na inchi zinazowazunguka. Kweli, wameyakataa maagizo yangu na kuacha kuyafuata masharti yangu.


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.


Kiburi cha Waisraeli kinawashuhudia wao wenyewe, hawanirudilii mimi Yawe, Mungu wao; wala hawanitafuti kwa ajili ya matukio hayo yote.


Tengeneza munyororo; kwa maana inchi imejaa makosa ya umwangaji wa damu na muji umejaa mateso makali.


Inua macho, uangalie vilele vya vilima! Kuna nafasi ambapo hawajalala nawe? Uliwangoja wapenzi wako kando ya njia, kama mubedui anavyovizia watu katika jangwa. Umeichafua inchi kwa ukahaba wako mubaya sana.


Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.


Hata hivyo, una haki kwa kutuazibu hivyo; maana wewe umekuwa mwaminifu wakati sisi tumekuwa watenda maovu.


Hata nyuma ya yote yaliyotupata kwa sababu ya maovu yetu na makosa yetu mengi, tunajua kwamba azabu uliyotupa, ee Mungu wetu, ni ndogo ikilinganishwa na makosa yetu, na umewaacha wazima wamoja kati yetu.


Lakini ninawaonya kwamba musipotimiza ahadi yenu, mutakuwa mumemutendea Yawe zambi; mujue kwa hakika kwamba mutaazibiwa.


Unihurumie, ee Mungu, kadiri ya wema wako; uyafute makosa yangu, kadiri ya wingi wa rehema yako.


Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Hivyo sheria haina nguvu, wala haki haifuatiliwi. Waovu wanawazunguka wenye haki, hivyo hukumu inatolewa na sheria imepotoshwa.


Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.


Ikiwa kuna watu walioponyoka, watakimbilia kwenye milima kama njiwa waliotishwa katika bonde. Kila mumoja wao ataomboleza kwa ajili ya zambi zake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite