Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 57:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Munafikiri kwamba munafanya sawa, lakini nitayafichua matendo yenu, nayo miungu yenu haitawafalia kitu.

Gade chapit la Kopi




Isaya 57:12
20 Referans Kwoze  

“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


Wanafanya matendo yao yote tu kusudi wajionyeshe mbele ya watu. Wanajifungia kwa paji za nyuso vibweta vipana vyenye vikaratasi vya Maandiko Matakatifu. Nao wanavaa kanzu zenye pembe ndefu.


Sisi wote tumekuwa kama watu wachafu; matendo yetu yote mema ni kama nguo chafu. Wote tunanyauka kama majani, uovu wetu unatupeperusha kama upepo.


Ole kwenu ninyi munaomuficha Yawe mipango yenu, munaotenda matendo yenu katika giza na kusema: Hakuna atakayetuona; nani anayeweza kujua tunachofanya?


Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Nitawalipiza maovu yao wayalipe vilevile maovu ya babu zao. –Ni Yawe anayesema hivyo.– Wao waliifukizia ubani miungu yao kwenye milima, wakanitukana mimi kule juu ya vilima. Nitawalipa sawa inavyostahili, watayalipa matendo yao ya zamani.


Ninayajua matendo yao na mawazo yao. Ninakuja kuwakusanya watu wa mataifa yote na wa luga zote, wakusanyike pamoja na kuuona utukufu wangu.


Watu wote wanaotengeneza sanamu za miungu ni bure kabisa; na vitu hivyo wanavyovifurahia haviwafalii kitu chochote. Wanaoshuhudia hiyo miungu ya uongo ni vipofu na wajinga. Kwa hiyo hao watafezeheshwa!


Basi, utawaambia hivi: Miungu hiyo ambayo haikuumba mbingu na dunia itaangamia. Itatoweka kabisa toka katika dunia, hapa chini ya mbingu.


Mwanadamu ni mujinga na mupumbafu; kila mufua zahabu anafezeheshwa na sanamu zake. Sanamu hizo ni uongo mutupu, hazina uzima wowote ndani yao.


Hazina faida, ni udanganyifu mutupu; wakati zitakapoazibiwa zote zitaangamia.


Hazina maana, ni udanganyifu mutupu; wakati watakapoazibiwa, nazo zitaangamia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite