Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 53:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Alionewa na kuteswa, lakini alivumilia kwa unyenyekevu, bila kutoa sauti hata kidogo. Alikuwa kama mwana-kondoo anayepelekwa kwenda kuchinjwa, kama kondoo anavyokaa kimya anapokatwa manyoya. Hakutoa sauti hata kidogo.

Gade chapit la Kopi




Isaya 53:7
17 Referans Kwoze  

Lakini Yesu akanyamaza. Kuhani Mukubwa akamwambia: “Ninakuapisha kwa jina la Mungu Mwenye Uzima, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”


Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.


Lakini Yesu akanyamaza, wala hakujibu neno. Kuhani Mukubwa akamwuliza tena: “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu mwenye sifa?”


Akaingia tena katika nyumba yake na kumwuliza Yesu: “Wewe ni muzaliwa wa wapi?” Lakini Yesu hakumujibu neno.


Akamwuliza Yesu maneno mengi, lakini yeye hakumujibu neno.


Lakini Yesu hakujibu neno lolote tena, hata Pilato akashangaa.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Halafu nikaona Mwana-Kondoo akisimama katikati ya kiti cha kifalme chenye kuzungukwa na vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee, naye alionekana kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba; ndizo roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote.


ee Mungu, ungalikwisha jua jambo hilo, kwa maana wewe unajua siri za moyo.


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


Nami nilikuwa kama kondoo mupole anayepelekwa kuchinjwa; sikujua kwamba shauri walilofanya lilikuwa juu yangu. Wao walisema: Tuuharibu muti pamoja na matunda yake, tumwue apate kusahaulika katika dunia, jina lake lisikumbukwe tena.


Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii; nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.


Kweli, nimekuwa kama mutu asiyesikia, kama mutu asiyekuwa na chochote cha kujitetea.


Wale walionipiga, niliwaelekezea mugongo wangu, wale walioziongoa ndevu zangu, mashavu yangu. Sikuficha uso wangu wakati watu waliponitukana na kunitemea mate.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite