Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 53:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.

Gade chapit la Kopi




Isaya 53:3
38 Referans Kwoze  

Halafu wamoja wakamutemea mate juu ya uso, na kumupiga ngumi. Na wengine wakamupiga makofi,


Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Akawaambia: “Ninahuzunika sana, karibu kufa! Mubakie hapa na mukeshe.”


Hata hivyo alitwaa mateso yetu, na kubeba huzuni zetu. Sisi tulifikiri amepata azabu, amepigwa na Mungu na kuteswa.


Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


Wale walionipiga, niliwaelekezea mugongo wangu, wale walioziongoa ndevu zangu, mashavu yangu. Sikuficha uso wangu wakati watu waliponitukana na kunitemea mate.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Naye akaongeza kuwaambia: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”


Wakati Wafarisayo waliposikia maneno haya yote wakamuzarau Yesu, kwa sababu walikuwa wapenda feza.


Nao wakamuchekelea kwa sababu walijua kwamba amekwisha kufa.


Wakamupigapiga tete juu ya kichwa, wakamutemea mate, wakapiga magoti na kuinama mbele yake.


Yesu akawajibu: “Hakika Elia anapaswa kurudi kwanza kutengeneza mambo yote. Lakini sababu gani Maandiko Matakatifu yanasema vilevile kwamba Mwana wa Mutu atateswa sana na kuzarauliwa?


Yesu akatoa machozi.


Wayuda wakamujibu: “Sisi tulikuwa na haki ya kusema kwamba wewe ni Musamaria na kwamba uko na pepo.”


na kumwambia: “Bwana, tunakumbuka kwamba wakati yule mudanganyifu alipokuwa angali muzima, alisema: ‘Kwa siku tatu kisha kufa kwangu, nitafufuka.’


Yawe anasema hivi: Lakini wewe Betelehemu katika Efurata, wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda, lakini kwako kutanitokea mutawala atakayetawala juu ya Israeli. Asili yake ni ya zamani sana.


Kwa muda wa mwezi mumoja, nikaua wachungaji watatu wabaya. Tena uvumilivu wangu kwa kondoo ukaniishia, nao kwa upande wao, wakanichukia.


Watu wa usawa walinona, wakapiga mateke. Walinenepa sana, kisha wakamwacha Mungu aliyewaumba, wakazarau Mulima wa wokovu wao.


Yesu alipokaribia muji wa Yerusalema, na alipouona, akaulilia,


Uwafute katika kitabu cha wenye kuishi, wasikuwe katika hesabu ya watu wa haki.


Akawaambia: “Tunapanda kwenda Yerusalema na kule Mwana wa Mutu atatolewa kwa wakubwa wa makuhani na kwa walimu wa Sheria. Nao watamuhukumu auawe na kumutoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine.


Nao watamuchekelea, watamutemea mate, watamupiga fimbo na kumwua. Lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”


Wengi waliomwona walishituka, kwa vile sura yake ilikuwa imeharibika; hakukuwa tena na umbo la mwanadamu!


Hasara inanipita kipimo, nami niko karibu kufa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite