Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 53:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Maana, mbele ya Yawe, mutumishi wake alikomaa kama kichipukizi, kama muzizi katika inchi kavu. Hakukuwa na umbo wala sura ya kupendeza, wala hakukuwa na uzuri wowote wa kutuvuta.

Gade chapit la Kopi




Isaya 53:2
22 Referans Kwoze  

Wengi waliomwona walishituka, kwa vile sura yake ilikuwa imeharibika; hakukuwa tena na umbo la mwanadamu!


Kutatokea chipukizi katika shina la Yese, tawi litachipuka toka mizizi yake.


Huyu si yule museremala, mwana wa Maria, ndugu ya Yakobo, Yose, Yuda na Simoni? Nao wadada zake, si wanaishi hapa kati yetu?” Na kwa hiyo wakakosa kumwaminia.


Siku zinakuja ambapo nitaotesha kichipukizi cha haki toka kizazi cha Daudi. Huyo atatawala kama mufalme, atatenda kwa hekima naye ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.


Yesu akawajibu: “Hakika Elia anapaswa kurudi kwanza kutengeneza mambo yote. Lakini sababu gani Maandiko Matakatifu yanasema vilevile kwamba Mwana wa Mutu atateswa sana na kuzarauliwa?


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


au ikiwa maliwali waliosimikwa naye kwa kuwaazibu watenda mabaya na kuwapa zawadi wale wanaotenda mema.


Basi Yesu akatoka inje, akivaa ile taji ya miiba na ile nguo nyekundu. Pilato akawaambia watu: “Mutu wenu huyu!”


Halafu wakalalamika kwa nguvu: “Hatutaki mutu huyu! Tunataka utufungulie Baraba!” (Yule Baraba alikuwa munyanganyi.)


Yesu akamwambia: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”


na kumwambia kwamba Yawe wa majeshi anasema hivi: Hapa kuna mutu anayeitwa Tawi. Yeye atastawi pale anapokuwa na kulijenga hekalu la Yawe.


Akazaa mwana, ndiye muzaliwa wake wa kwanza. Akamufunika nguo za kitoto na kumulalisha katika sanduku ya kukulishia nyama, kwa sababu walikosa nafasi ya kukaa katika nyumba ya kupangisha wageni.


Siku ile, tawi Yawe atakalochipuza litakuwa zuri na tukufu, nayo matunda ya inchi yatakuwa na heshima na utukufu kwa wale Waisraeli watakaobaki. Waisraeli watakaobaki watasifiwa na kujivunia mazao ya inchi yao.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Sasa sikiliza kwa uangalifu, ewe Yoshua, Kuhani Mukubwa; musikilize vilevile enyi makuhani wenzake munaokuwa pamoja naye, ninyi munaokuwa kitambulisho cha wakati muzuri unaokuja: Nitamuleta mutumishi wangu anayeitwa Tawi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite