Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 53:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ni nani aliyeamini mambo tuliyoyasikia? Mukono wa Mungu umefunuliwa kwa ajili ya nani?

Gade chapit la Kopi




Isaya 53:1
16 Referans Kwoze  

kusudi maneno haya yaliyosemwa na nabii Isaya yatimie: “Bwana, ni nani aliyeamini habari tuliyopasha? Nani aliyefunuliwa matendo ya uwezo ya Bwana?”


Hivi, mahubiri ya kufa kwa Kristo juu ya musalaba yanahesabiwa kuwa upumbafu kwa wale wanaopotea. Lakini kwa sisi tunaookolewa ni uwezo wa Mungu.


Lakini wamoja waliomupokea, ndio wale waliomwamini, aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu.


Halafu Yesu akamwambia: “Heri kwako, wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana hakuna mutu aliyekufunulia neno hili isipokuwa Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Lakini kwa wale walioitwa na Mungu, ikiwa Wayuda au wasiokuwa Wayuda, Kristo ni kitambulisho cha uwezo na hekima ya Mungu.


Kisha utukufu wa Yawe utafunuliwa, na watu wote pamoja watauona. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?


Alikuja kushuhudia ule mwangaza kusudi watu wote wapate kuamini kwa njia yake.


Yawe ameapa kwa uwezo wake mukubwa, ameapa kwa nguvu yake akisema: Sitawapa tena waadui zako ngano yako; wala wageni hawatakunywa tena divai yako ambayo umeitoshea jasho.


Halafu Yesu akawatwaa wanafunzi wake kumi na wawili pembeni, akawaambia: “Tunapanda kwenda Yerusalema, na maneno yote yaliyoandikwa na manabii juu ya Mwana wa Mutu yatatimizwa.


Aliona kwamba hakuna mutu aliyejali, akashangaa kwamba hakuna aliyeingilia kati. Basi akaamua kunyoosha mukono wake mwenyewe, haki yake ikamusaidia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite