Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 51:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe anasema hivi: Munisikilize enyi munaotaka kukombolewa, ninyi munaonitafuta mimi Yawe. Muangalie jiwe mulilochongwa toka ndani yake, mulima mulimochimbuliwa.

Gade chapit la Kopi




Isaya 51:1
29 Referans Kwoze  

Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.


Maana hukumu zitatolewa kwa haki tena, na wote wenye moyo wa usawa watazifuata.


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


Basi kwa hiyo tujikaze sana kufanya mambo yale yanayoleta amani na yanayotusaidia kujengana katika imani.


Unisikilize ee taifa la Yakobo, unisikilize ee Israeli niliyekuita. Mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi.


Mutafute Yawe, nanyi mutaishi! Kama sivyo, atawatokea wazao wa Yosefu kama moto; moto utawateketeza wakaaji wa Beteli na hakuna mutu atakayeweza kuuzimisha.


Anayetafuta haki na wema atapata uzima, haki, na heshima.


Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini Mungu anawapenda wale wanaofuata mambo ya haki.


Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.


Wandugu zangu, sihesabu kwamba nimekwisha kupokea zawadi, lakini ninafanya jambo moja tu: ninasahau yanayokuwa nyuma, nikifukuzia yanayokuwa mbele yangu.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!


Mimi sikusema kwa siri, wala katika inchi yenye giza. Mimi sikuwaambia wazao wa Yakobo wanitafute pahali kusipokuwa kitu. Mimi Yawe ninasema ukweli, maneno yangu ni ya kuaminika.


Ndiyo hali ya kizazi cha watu wanaomutafuta yeye, watu wanaomutafuta Mungu wa Yakobo.


Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.


Mumutafute Yawe wakati angali anaweza kupatikana, mumwombe musaada wakati angali karibu.


Munisikilize, enyi watu wangu, munitegee sikio, enyi taifa langu. Sheria na haki zitatoka kwangu mimi; nazo zitakuwa mwangaza wa mataifa.


Hawakufahamu namna Mungu anavyowahesabia watu haki na wakatafuta kusimamisha haki yao wenyewe. Wakakataa kufuata njia ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


Bonde la Saroni litakuwa nafasi ya kukulishia nyama, bonde la Akori litakuwa mapumziko ya ngombe kwa ajili ya watu wangu walionitafuta.


naye akatoka kwenda kukutana na mufalme Asa, akamwambia: “Unisikilize, ee Asa na watu wote wa kabila la Yuda na la Benjamina! Yawe yuko pamoja nanyi, ikiwa mutakuwa pamoja naye. Mukimutafuta, mutamupata, lakini mukimwacha, naye atawaacha.


Lakini walipopatwa na shida, walimugeukia Yawe, Mungu wa Israeli, wakamutafuta, wakamupata.


Musikilize, enyi watu wa Yakobo, enyi munaojulikana kwa jina la Israeli, ninyi munaokuwa wa uzao wa Yuda. Ninyi munaapa kwa jina la Yawe, na kudai kwamba munamwabudu Mungu wa Israeli; lakini hayo si ukweli wala sawa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite