Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 5:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Kwa ajili ya kituliro kidogo wanawaachilia wenye kosa na kuwanyima wasiokuwa na kosa haki yao.

Gade chapit la Kopi




Isaya 5:23
22 Referans Kwoze  

Wanakataa kusambisha wazaifu, wananyanganya watu wangu wamasikini haki yao. Wanateka wajane; wananyanganya wayatima mali yao.


Mumewahukumu na kuwaua wenye haki, nao hawakupingana nanyi.


Kumuhesabu mwovu kuwa na haki na kumwazibu asiyekuwa na kosa, yote mawili ni chukizo kwa Yawe.


Wao wanapatana kuwaangamiza watu wa haki, na kuwahukumu watu wasiokuwa na kosa wauawe.


Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.


Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!


Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Anayemwachilia mutu mwenye kosa analaaniwa na watu na kuchukiwa na mataifa.


Mutu mubaya anapokea kituliro kwa siri kusudi apate kupotosha haki.


Basi, sasa mumwogope Yawe, mukuwe waangalifu katika kila jambo mutakalotenda kwa sababu Yawe wetu hatavumilia upotoshaji wa haki, wala upendeleo wala upokeaji wa kituliro.”


Musipotoshe haki, musikuwe na upendeleo, wala musikubali kupokea kituliro, kwa kuwa kituliro kinapofusha macho ya watu wenye hekima na kupotosha maneno ya mutu mwenye haki.


Na hivi mutabeba lazima ya damu iliyomwangwa katika dunia pasipo kosa, tangia kuuawa kwa Abeli aliyekuwa mukamilifu mpaka kuuawa kwa Zakaria, mwana wa Barakia, muliyemwuia kwenye hekalu katikati ya Pahali Patakatifu na mazabahu.


Wale watenda maovu wawili wakaikaa kwa kumushuhudia Naboti, kisha wakamushitaki mbele ya watu wote wakisema: “Naboti amemutukana Mungu na mufalme.” Basi, Naboti akapelekwa inje ya muji, akauawa kwa kutupiwa mawe.


Ole kwao wanaotunga sheria za uovu, watu wanaopitisha sheria za kugandamiza.


Matendo ya watu wadanganyifu ni mabaya; hao wanatunga maneno mabaya kwa kumwangamiza masikini kwa maneno ya uongo, hata kama masikini ni mwenye sheria.


Ukweli umekosekana, naye anayeacha uovu ananyanganywa. Mungu aliona mambo hayo. Alichukizwa kwamba watu hawafuati sheria yake.


Maana mimi ninajua wingi wa makosa yenu na ukubwa wa zambi zenu; ninyi munawatesa watu wema, munapokea kituliro na kuzuia wakosefu wasipate haki katika tribinali.


Lakini kuna wengine waliolewa divai na kuyumbayumba kwa sababu ya pombe kali; makuhani na manabii wamelewa pombe kali, wamevurugika kwa divai. Wanayumbayumba kwa pombe kali; maono yao yamepotoka, wanajikwaa katika kutoa hukumu.


Watatoweka wale wanaopotosha maneno ya mutu katika tribinali, watu wanaowatega waamuzi na wanaosema uongo kwa kuwanyima haki yao wasiokuwa na kosa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite