Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 5:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Ole kwao wanaokuwa wafundi wa kunywa divai, wanaokuwa hodari sana wa kuchanganya vinywaji vya kulewesha.

Gade chapit la Kopi




Isaya 5:22
14 Referans Kwoze  

Ole kwao wanaoamuka asubui mapema wapate kukimbilia kinywaji cha kulewesha; wanaokesha hata usiku, mpaka divai iwaleweshe!


Ole wako unayewalewesha jirani zako, na kutia sumu katika divai yao kusudi upate kuwaona wakiikaa uchi.


Lakini kuna wengine waliolewa divai na kuyumbayumba kwa sababu ya pombe kali; makuhani na manabii wamelewa pombe kali, wamevurugika kwa divai. Wanayumbayumba kwa pombe kali; maono yao yamepotoka, wanajikwaa katika kutoa hukumu.


Wao wanaambiana hivi: Mukuje, tuende kutafuta divai; mukuje tukunywe tushibe kinywaji kikali! Kesho itakuwa kama leo, tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.


Usipokee kituliro, maana kituliro kinapofusha wakubwa na kupotosha mambo ya wenye haki.


Divai inaleta mazarau na kileo kinaleta ugomvi; yeyote anayevutwa navyo hana hekima.


Ni nani wenye taabu? Ni nani wenye huzuni? Ni nani wenye ugomvi? Ni nani wenye malalamiko? Ni nani wenye vidonda bila sababu? Ni nani wenye macho mekundu?


Haifai, ee Lemueli, haifai wafalme kunywa divai, wala wakubwa kutamani vileo.


Lakini ninyi mukafurahi na kusherehekea. Mulichinja ngombe na kondoo, mukakula nyama na kunywa divai. Ninyi mulisema: Acha tukule na kunywa maana kesho tutakufa.


Hakuna tena kunywa divai na kuimba; kinywaji cha kulewesha kimekuwa uchungu kwa wakunywaji.


Basi, wakati wa saa sita za muchana, Beni-Hadadi na wale wafalme wenzake makumi tatu na wawili waliomwunga mukono walipokuwa katika mahema yao wakikunywa na kulewa, mashambulizi yakaanza.


Wakikunywa watasahau maagizo ya sheria, na kuwanyima haki wenye taabu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite