Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 5:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Shamba la mizabibu lenye hektari kumi litatoa litre makumi tano tu za divai; anayepanda kilo mia moja za mbegu atavuna kilo kumi tu.

Gade chapit la Kopi




Isaya 5:10
13 Referans Kwoze  

Chakula chenu nitakipunguza hata wanawake kumi watumie mafika moja tu kwa kupika mikate. Watawagawanyia mukate wenu kwa kipimo. Na hata kisha kula mutaendelea kuwa na njaa tu.


hali yenu ilikuwa namna gani? Mutu alifika kwenye fungu la ngano akingojea kupata vipimo makumi mbili, lakini kulikuwa vipimo kumi tu. Mutu alifika kwenye mutungi wa divai akingojea kujaza vyombo makumi tano, lakini kulikuwa makumi mbili tu.


Munapanda mbegu kwa wingi, lakini munavuna kidogo. Munakula, lakini hamushibi. Munakunywa divai, lakini hamutosheki. Munavaa nguo, lakini bado munasikia baridi. Mushahara wa mutumishi unakuwa kama umetumbukizwa katika mufuko uliotoboka.


Mbegu zinaoza ndani ya udongo; gala zimebaki bila kitu, vibanda vya kuwekea mavuno vimebomoka, kwa maana hakuna tena ngano.


Mutu akitakasa shamba lake, ambalo ni urizi wake, kwa ajili ya Yawe, basi, bei yake itapimwa kulingana na mbegu zinazotumiwa kwa kupanda shamba hilo. Kwa kila kilo makumi mbili za shayiri bei yake itakuwa shekeli makumi tano za feza.


Mutapanda mbegu nyingi lakini mutavuna kidogo tu kwa sababu nzige watakula mazao yenu.


Mutapanda mizabibu na kuitunza, lakini hamutavuna mizabibu hiyo wala kunywa divai yake, maana wadudu wataikula.


Wakati huo, kila pahali palipokuwa mizabibu elfu moja iliyopata vikoroti vya feza elfu moja, patakuwa michongoma na miiba mitupu.


juu ya inchi ya watu wangu inayoota miiba na michongoma, juu ya nyumba zote zilizojaa watu wenye furaha, juu ya muji uliokuwa na shangwe.


Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka inchi ya Moabu yenye mboleo. Nimeikomesha divai kutoka katika vikamulio. Hakuna mutu anayekamua mizabibu kwa shangwe; kelele zinazosikilika si za shangwe.


Vifundo hivyo na matawi vilikuwa kitu kimoja na kinara hicho na chote kilifuliwa kwa zahabu safi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite