Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 48:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kwa heshima ya jina langu, ninatuliza hasira yangu; kwa ajili ya heshima yangu, ninajizuiza kusudi nisikuangamize.

Gade chapit la Kopi




Isaya 48:9
22 Referans Kwoze  

Ulinde uzima wangu, ee Yawe, kwa ajili ya jina lako, uniondoe katika taabu, kwa ajili ya haki yako.


Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi, kusudi aonyeshe nguvu yake kubwa.


Utusaidie, ee Mungu, mwokozi wetu kwa utukufu wa jina lako. Utuokoe na kutusamehe zambi zetu, kwa ajili ya jina lako.


Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, wala hakuwaangamiza. Mara nyingi alizuia hasira yake, wala hakuacha kasirani yake yote iwake.


Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe, wakati nitakapowatendea ninyi sio kulingana na mwenendo wenu na matendo yenu mabaya, lakini kwa heshima ya jina langu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Lakini nilizuiza mukono wangu kwa sababu ya heshima ya jina langu kusudi nisizarauliwe kati ya watu wa mataifa walioona nikiwatoa katika inchi ya Misri.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa ambao waliona jinsi nilivyowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Ninafanya hivyo kwa ajili yangu mwenyewe. Kwa nini jina langu lizarauliwe? Siwezi kumupatia mwingine utukufu wangu!


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Kwa ajili ya jina lako, ee Yawe, unisamehe kosa langu, kwa maana ni kubwa.


Kwa heshima ya jina lake kubwa, Yawe hatawatupa watu wake kwa sababu amependa kuwafanya ninyi mukuwe watu wake.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.


Mwenye akili hakasiriki upesi; kusamehe makosa ni utukufu kwake.


Basi, Wakanana pamoja na wakaaji wote wa inchi hii watakapopata habari hiyo watatuzunguka na kutufuta kabisa katika dunia. Sasa utafanya nini kwa kuonyesha ukubwa wa jina lako?”


Yawe anasema hivi: Mutu akikuta kishada cha mizabibu mizuri, watu wanasema: Tusikiharibu; kina baraka. Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.


Hiyo ilinifanya kuhangaika juu ya jina langu takatifu ambalo Waisraeli walilikufuru kati ya mataifa walikokwenda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite