Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 48:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Unisikilize ee taifa la Yakobo, unisikilize ee Israeli niliyekuita. Mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.

Gade chapit la Kopi




Isaya 48:12
28 Referans Kwoze  

Nani aliyefanya yote haya yatendeke? Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio? Mimi Yawe nipo tangu mwanzo, mimi nitakuwa hata milele.


Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho.”


Bwana Mungu Mwenye Uwezo anasema: “Mimi ni Alfa na Omega.” Ni yeye anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja.


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Mimi peke yangu ndiye Yawe, hakuna mukombozi mwingine isipokuwa mimi.


Munisikilize, enyi inchi za mbali, Mutege sikio, enyi watu wa mbali! Yawe aliniita mbele sijazaliwa, alitaja jina langu nikiwa katika tumbo la mama yangu.


Musikilize, enyi wazao wa Yakobo, munisikilize, enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli. Mimi niliwatunza ninyi tangu mulipozaliwa; niliwabeba ninyi tangu katika tumbo la mama yenu.


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”


“Umwandikie malaika wa kanisa la Smurna hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa lakini sasa ni muzima.


ikisema: “Andika katika kitabu mambo unayoona, na ukitume kwa makanisa ya miji saba: Efeso, Smurna, Pergamo, Tuatera, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Lakini kwa wale walioitwa na Mungu, ikiwa Wayuda au wasiokuwa Wayuda, Kristo ni kitambulisho cha uwezo na hekima ya Mungu.


Tunajua kwamba katika mambo yote Mungu anatumika kwa kuwajalia wale wanaomupenda, ndio wale walioitwa naye kufuatana na kusudi lake.


Nanyi vilevile munakuwa kati ya watu wale; mumeitwa na Mungu mukuwe watu wa Yesu Kristo.


Yesu akaongeza kusema: “Ni hivi inavyokuwa vilevile: wanaokuwa wa mwisho watakuwa wa kwanza, nao wanaokuwa wa kwanza watakuwa wa mwisho.”


Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.


Munisikilize, enyi watu wangu, munitegee sikio, enyi taifa langu. Sheria na haki zitatoka kwangu mimi; nazo zitakuwa mwangaza wa mataifa.


Yawe anasema hivi: Munisikilize enyi munaotaka kukombolewa, ninyi munaonitafuta mimi Yawe. Muangalie jiwe mulilochongwa toka ndani yake, mulima mulimochimbuliwa.


Mujongee musikilize enyi mataifa, musikilize enyi watu. Sikiliza, ee dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, ulimwengu na vyote vinavyotoka humo!


“Sasa basi, wana wangu, munisikilize: heri wale wanaofuata njia zangu.


Sasa wana wangu, munisikilize; mutege sikio kwa maneno ya kinywa changu.


Muinue macho yenu juu mbinguni! Ni nani aliyeziumba nyota hizo? Ni yule anayeziongoza kama jeshi lake, anayeijua hesabu yake yote, anayeziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi, hakuna hata moja inayokosekana.


Ninyi Waisraeli ni washuhuda wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwachagua mukuwe watumishi wangu, mupate kunijua na kuniamini, kwamba mimi ni Mungu. Mbele yangu hakukuwa mungu mwingine, wala hakutakuwa mungu mwingine nyuma yangu.


Mimi nitabaki yuleyule hata katika uzee wenu; hata katika wakati wenu wa imvi mimi nitawabeba. Nilifanya hivyo kwanza, nitafanya hivyo tena. Nitawabeba ninyi na kuwaokoa.


Sikiliza, ewe Israeli, mutumishi wangu; sikiliza, enyi wazao wa Yakobo, muchaguliwa wangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite