Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 48:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Ninafanya hivyo kwa ajili yangu mwenyewe. Kwa nini jina langu lizarauliwe? Siwezi kumupatia mwingine utukufu wangu!

Gade chapit la Kopi




Isaya 48:11
23 Referans Kwoze  

Jina langu mimi ni Yawe; sitamupa mwingine utukufu wangu, wala sifa zangu sanamu za miungu.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa ambao waliona jinsi nilivyowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.


Lakini nilizuiza mukono wangu kwa sababu ya heshima ya jina langu kusudi nisizarauliwe kati ya watu wa mataifa walioona nikiwatoa katika inchi ya Misri.


Kwa heshima ya jina lake kubwa, Yawe hatawatupa watu wake kwa sababu amependa kuwafanya ninyi mukuwe watu wake.


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe, wakati nitakapowatendea ninyi sio kulingana na mwenendo wenu na matendo yenu mabaya, lakini kwa heshima ya jina langu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Na sasa, enyi Waisraeli, Bwana wenu Yawe anawaambia hivi: Muendelee kuziabudu sanamu zenu za miungu, kama hamunisikilizi; lakini mutalazimishwa kuacha kulikufuru jina langu takatifu kwa sadaka na sanamu zenu.


Kwa maana kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu yenu, jina la Mungu linatukaniwa katikati ya watu wa mataifa mengine.”


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


Katika hali ya sasa ninapata faida gani kuwaona watu wangu wamepelekwa katika utumwa? –Ni ujumbe wa Yawe. Hao wanaowatawala wanajitapa. Nalo jina langu linaendelea kuzarauliwa kila siku. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa hiyo nilikutangazia mambo yale tangu zamani, mbele hayajatukia, mimi nilikujulisha, kusudi usiseme: Ni sanamu yangu iliyotenda mambo hayo, sanamu zangu za chuma ndizo ziliyaagiza.


Kwa ajili ya jina lako, ee Yawe, unisamehe kosa langu, kwa maana ni kubwa.


Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi, kusudi aonyeshe nguvu yake kubwa.


Si sisi, ee Yawe, si sisi; lakini wewe peke yako utukuzwe, kwa ajili ya wema na uaminifu wako.


Kwa heshima ya jina langu, ninatuliza hasira yangu; kwa ajili ya heshima yangu, ninajizuiza kusudi nisikuangamize.


Kwa hiyo, ee Mungu, usikilize malalamiko yangu na maombi yangu mimi mutumishi wako. Kwa ajili ya heshima yako, ulionee tena hekalu lako lililoharibika huruma.


Usikumbuke zambi na makosa ya ujana wangu; unikumbuke kwa kadiri ya wema wako, kwa ajili ya uzuri wako, ee Yawe.


Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninachotaka kufanya si kwa faida yenu ninyi watu wa inchi ya Israeli, lakini ni kwa heshima ya jina langu takatifu mulilolikufuru kati ya mataifa mulikokwenda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite