Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 47:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Haya yote mawili yatakupata kwa rafla katika siku moja: kupoteza watoto wako na kuwa mujane, ijapokuwa una wingi wa uchawi wako, na nguvu nyingi za uganga wako.

Gade chapit la Kopi




Isaya 47:9
26 Referans Kwoze  

Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Wanaangamizwa kwa rafla, wateketezwe kabisa kwa vitisho.


Ninawe! Wewe umekuwa kama kahaba. Umewashawishi watu, ewe binti wa uchawi, uliyeyafanya mataifa kuwa watumwa kwa ukahaba wako, na watu wa mataifa kwa uchawi wako.


Lakini mbali ya muji ule kuna watu wenye kuchukiza, wachawi, wazinzi, wauaji, wanaobudu sanamu na wasema uongo na wote wanaoupenda.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.


Nilipokuwa ninalala, niliona maono haya: Niliona muti murefu sana katikati ya dunia.


Basi, mufalme akaamuru waganga, walozi na wachawi wa Wakaldea waletwe kusudi wamufasirie ndoto yake. Wote wakakuja na kusimama mbele yake.


Inchi inatetemeka na kugaagaa kwa maumivu, maana nia ya Yawe juu ya Babeli ni imara: ataifanya inchi ya Babeli kuwa jangwa, ataifanya ikuwe bila watu.


Naomi akasema: “Musiniite tena Naomi muniite Mara, kwa maana Mungu Mwenye Nguvu ameyafanya maisha yangu yakuwe machungu sana.


Malona na Kiliona nao vilevile wakakufa.


Watoto wao wachanga watapondwapondwa mbele yao, watanyanganywa nyumba zao, na watalala na wake zao kwa kinguvu.


Angalia, wanakuja: waaskari wapanda-farasi wawiliwawili. Wanasema: Babeli umeanguka! Umeanguka! Sanamu zote za miungu yake zimetupwa chini na kuvunjwavunjwa!


Lakini hasara itakupata ambayo hautaweza kujiepusha nayo. Magumu yatakutokea ambayo hautaweza kuyapinga; maangamizi yatakufikia kwa rafla ambayo haujapata kuyaona hata kidogo.


Mama aliyeheshimiwa kwa kuwa na watoto saba, sasa kwa rafla hana kitu. Amezimia na kukata roho, amekufa angali kijana, amefezeheka na kuzarauliwa. Na wale watakaobaki wazima nitawatoa kwa upanga mbele ya waadui zao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Usiku uleule, mufalme Belsasari wa Wakaldea, aliuawa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite