Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 43:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Musiogope maana mimi nipo pamoja nanyi. Nitawarudisha wazao wenu toka mashariki, nitawakusanya ninyi kutoka magaribi.

Gade chapit la Kopi




Isaya 43:5
41 Referans Kwoze  

hapo Yawe, Mungu wenu, atawarudishia mema yenu na kuwahurumia na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa ambamo atakuwa amewatawanya.


Watu watakuja toka mashariki na magaribi, kaskazini na kusini, nao wataikaa kula chakula katika Ufalme wa Mungu.


Watu wangu watarudia kutoka mbali, wengine kutoka kaskazini na magaribi, wengine kutoka upande wa kusini.


Mimi, Yawe Muumba wako, niliyekutengeza tangia tumbo la mama yako, ninakuja kukusaidia wewe. Mimi Yawe ninasema hivi: Musiogope, enyi wazao wa Yakobo, mutumishi wangu, usiogope, ewe Yeshuruni, muchaguliwa wangu.


Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


Yawe anasema hivi: Nitawaokoa watu wangu kutoka inchi ya mashariki na kutoka inchi ya magaribi


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Sikiliza ewe Israeli, mutumishi wangu, wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua, wewe wa uzao wa Abrahamu, rafiki yangu;


Utuokoe, ee Yawe, Mungu wetu, utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa, tupate kusifu jina lako takatifu, na kuona utukufu juu ya sifa zako.


Niko na kondoo wengine wasiokuwa wa kundi hili. Ninapaswa vilevile kuwaleta, nao watasikia sauti yangu, na kutakuwa kundi moja na muchungaji mumoja.


Lakini kweli nitawakusanya ninyi wote enyi watu wa Yakobo, nitawakusanya enyi Waisraeli muliobaki, niwalete pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi kubwa la kondoo katika shamba la malisho; nanyi mutakuwa kundi la watu wengi.


akawakusanya kutoka inchi za kigeni: kutoka mashariki na magaribi, kutoka kaskazini na kusini.


Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure; mufanye mipango lakini haitawezekana, maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.


wewe niliyekuleta toka miisho ya dunia, niliyekuita toka mbali kwa mipaka ya dunia, wewe niliyekuambia: Wewe ni mutumishi wangu; mimi sikukutupilia, lakini nilikuchagua.


Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.


Inua macho uangalie pande zote; watu wako wote wanakusanyika na kukufikia. Kama vile ninavyoishi, watu wako watakuwa kwako kama mapambo, utawafurahia kama vile bibi arusi anavyofanya na taji lake. –Ni ujumbe wa Yawe.


maana utapanuka kila upande; wazao wako watarizi mataifa, miji iliyokuwa ukiwa itajaa watu.


Nilikuacha kwa muda mufupi tu. Kwa huruma nyingi, nitakurudisha.


Wazao wao watajulikana kati ya mataifa; watajulikana kati ya watu wengine. Kila mutu atakayewaona atakubali kwamba wao ni watu waliobarikiwa na Yawe.


Lakini wataapa wakisema: Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyewaondoa na kuwaongoza Waisraeli kutoka inchi ya kaskazini na kutoka inchi zote ambapo alipowafukuza. Na halafu wataishi katika inchi yao wenyewe. –Ni ujumbe wa Yawe.


mutaniona. Nitatengeneza upya maisha yenu na kuwakusanya kutoka mataifa yote na pahali pote nilipowasambaza. Nitawarudisha pahali nilipowaondoa wakati nilipowapeleka katika uhamisho. –Ni ujumbe wa Yawe.


Musimwogope mufalme wa Babeli munayemwogopa; musimwogope hata kidogo. Mimi niko pamoja nanyi kwa kuwaokoa na kuwaponyesha kutoka katika mikono yake.


Musiregee wala musikuwe na hofu, kwa sababu ya habari munazosikia katika inchi. Mwaka huu kuna habari hii, mwaka mwingine habari ingine; habari ya mateso makali katika inchi, mutawala mumoja anapigana na mutawala mwingine.


Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika inchi ya kaskazini na kurudi katika inchi niliyowapa babu zenu ikuwe urizi wao.


Kwa hiyo, siku zinakuja siku ambapo watu hawataapa tena, wakisema: Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyewaondoa watu wa Israeli kutoka katika inchi ya Misri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite