Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 42:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yeye hataregea wala kuchoka, mpaka atakapoimarisha sheria yangu katika dunia. Watu wa mbali wanangojea mafundisho yake.

Gade chapit la Kopi




Isaya 42:4
33 Referans Kwoze  

Sasa utayaita mataifa usiyoyajua, watu wa mataifa yasiyokutambua watakuja mbio kwenu, kwa sababu yangu mimi Yawe, Mungu wako; kwa sababu yangu mimi Mutakatifu wa Israeli niliyekufanya wewe upate utukufu.


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Nayo mataifa yote yatamutumainia.”


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Wamasikini watakula na kushiba; wanaomutafuta Yawe watamusifu. Mungu awajalie waishi milele!


Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!


Nitaweka kati yao kitambulisho cha uwezo wangu. Watakaookolewa kati yao nitawapeleka kwa watu wa mataifa kule Tarsisi, Puti, Ludi, inchi zenye wafundi wa kupiga upinde; watakwenda vilevile Tubali na Ugriki na katika visanga vya mbali ambapo watu hawajapata kusikia habari zangu wala kuuona utukufu wangu. Wale wajumbe wangu watautangaza utukufu wangu katika mataifa hayo.


Ni mashua zinazotoka katika inchi za mbali, zikitanguliwa na mashua za Tarsisi. Zinawaleta watoto wako, pamoja na feza na zahabu yao, kwa sifa ya Yawe, Mungu wako, kwa sifa ya Mungu, Mutukufu wa Israeli, maana amewafanya mupate utukufu.


Wote wanaokaa katika inchi za mbali, wamutukuze na kumusifu Yawe.


Vilevile ninapokuwa kati ya wasioishi chini ya Sheria ya Musa, ninaishi kama wao, bila kuangalia Sheria, kusudi niwapate. Hii si kusema kwamba mimi sishiki sheria ya Mungu, kwa maana mimi ni chini ya uongozi wa sheria ya Kristo.


Lakini sasa yamefunuliwa na maandiko ya manabii kufuatana na amri ya Mungu wa milele, kusudi mataifa yote yapate kumwamini na kumutii.


Munisikilize, enyi inchi za mbali, Mutege sikio, enyi watu wa mbali! Yawe aliniita mbele sijazaliwa, alitaja jina langu nikiwa katika tumbo la mama yangu.


Wakaaji wa mbali wameona mambo niliyotenda, wakaogopa; dunia yote inatetemeka kwa woga. Watu wote wamekusanyika, wakakuja.


Ninyi hamujui bado? Hamujapata kusikia? Yawe ndiye Mungu wa milele; yeye ndiye Muumba wa kila kitu katika dunia. Yeye haregei hata kidogo wala kuchoka. Maarifa yake hayachunguziki.


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Dunia yote iimbe sifa zake: bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, inchi za mbali na wakaaji wake;


Kwa ajili ya uaminifu wake, Yawe, alipenda kutukuza sheria yake na kuiheshimisha.


Munisikilize, enyi watu wangu, munitegee sikio, enyi taifa langu. Sheria na haki zitatoka kwangu mimi; nazo zitakuwa mwangaza wa mataifa.


Ukombozi wangu unakaribia upesi; wokovu nitakaoleta unaanza kutokea. Mimi mwenyewe nitayatawala mataifa. Wakaaji wa inchi za mbali wananingojea, wanaitegemea nguvu yangu.


Dunia iliumbwa na yule anayeikaa juu ya mbingu; kutoka huko wakaaji wa dunia ni kama mapanzi! Yeye ametandika mbingu kama pazia, na kuzikunjua kama hema la kuishi ndani yake.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Halafu Yesu akamwambia yule mwenye mukono unaokauka: “Simama hapa katikati.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite