Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 41:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Nani aliyefanya yote haya yatendeke? Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio? Mimi Yawe nipo tangu mwanzo, mimi nitakuwa hata milele.

Gade chapit la Kopi




Isaya 41:4
26 Referans Kwoze  

Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho.”


Unisikilize ee taifa la Yakobo, unisikilize ee Israeli niliyekuita. Mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Wakati nilipomwona, nikaanguka chini kwa rafla mbele yake kama vile mufu. Lakini akaweka mukono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Nani aliyetangaza haya tangu mwanzo, hata sisi tupate kuyatambua? Nani aliyetangulia kuyatangaza, kusudi sasa tuseme, alisema ukweli? Hakuna hata mumoja kati yenu aliyeyataja, wala hakuna aliyesikia maneno yenu.


Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo, tangu zamani nilitangaza mambo yatakayotukia. Kusudio langu litatimia; mimi nitatimiza nia yangu yote.


Ninyi Waisraeli ni washuhuda wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwachagua mukuwe watumishi wangu, mupate kunijua na kuniamini, kwamba mimi ni Mungu. Mbele yangu hakukuwa mungu mwingine, wala hakutakuwa mungu mwingine nyuma yangu.


Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.


Bwana Mungu Mwenye Uwezo anasema: “Mimi ni Alfa na Omega.” Ni yeye anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja.


Ni nani aliyewatia Waisraeli katika mikono ya waadui zao? Nani aliyewaacha wanyanganywe mali zao? Ni Yawe ambaye tumemukosea! Wazee wetu walikataa kuzifuata njia zake, wala hawakuzitii amri zake.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Smurna hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa lakini sasa ni muzima.


ikisema: “Andika katika kitabu mambo unayoona, na ukitume kwa makanisa ya miji saba: Efeso, Smurna, Pergamo, Tuatera, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”


Ni nani anayeweza kupima maji ya bahari katika kitanga cha mukono wake, na kuzipima mbingu kwa mikono yake? Ni nani anayeweza kuutia udongo wa dunia katika kikombe; kuipima milima kwa mizani au vilima kwa kipimo cha uzito?


Ni vile Bwana anavyosema, yeye aliyejulisha mambo haya tangu zamani za kale.’ ”


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


Muinue macho yenu juu mbinguni! Ni nani aliyeziumba nyota hizo? Ni yule anayeziongoza kama jeshi lake, anayeijua hesabu yake yote, anayeziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi, hakuna hata moja inayokosekana.


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Vitatoweka na kuchakaa kama nguo, lakini wewe utabaki. Utavibadilisha kama nguo, navyo vitapita.


Yeye anawakimbiza na kupita kwa usalama; anaenda mbio bila kukanyaga chini.


Mimi ni Mungu na nitakuwa Mungu siku zote. Hakuna anayeweza kuepuka nguvu yangu; hakuna anayeweza kupinga ninayofanya.


Lakini wewe unabaki sawasawa, na maisha yako hayana mwisho.


Watu wataona jambo hilo, nao watatambua na kuelewa kwamba mimi Yawe nimetenda hayo, mimi Mutakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite