Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 41:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.

Gade chapit la Kopi




Isaya 41:10
63 Referans Kwoze  

Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.


Lakini akanijibu: “Neema yangu inakutoshelea, kwa maana uwezo wangu unatimizwa katika uzaifu.” Basi tafazali nijivunie sana uzaifu wangu kusudi nijazwe na uwezo wa Kristo.


Zaburi ya Daudi. Yawe ni mwangaza wangu na wokovu wangu, ni nani nitakayemwogopa? Yawe ni mulinzi wa maisha yangu, sitamwogopa mutu yeyote.


maana wewe umenisaidia siku zote. Nitashangilia chini ya kivuli cha mabawa yako.


Hamutahitaji kupigana vita hivi. Ninyi mujipange tu halafu mungojee, na mutaona Yawe akiwashinda kwa jina lenu. Enyi watu wa Yuda na Yerusalema, musiogope wala musifazaike. Muende kwa vita, naye Yawe atakuwa pamoja nanyi!”


Yawe anawashikilia wote wanaoanguka; anawainua wote waliogandamizwa.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Hautahitaji tena jua kukuangazia muchana, wala mwezi kukuangazia usiku; maana mimi Yawe ni mwangaza wako milele; mimi Mungu wako nitakuwa utukufu wako.


“Mukienda kwa vita kupigana na waadui zenu, mukiona farasi, magari na jeshi kubwa zaidi kuliko lenu musiwaogope. Maana Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa Misri, atakuwa nanyi.


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Hata akianguka, hatabaki chini, kwa sababu Yawe anamuimarisha.


Yawe awape watu wake nguvu! Yawe awabariki watu wake kwa amani!


Ninaomba Mungu, kwa uwingi wa utukufu wake, awajalie nguvu mupate kuwa imara ndani ya roho zenu, kwa njia ya Roho wake.


Yeye ana nguvu za kibinadamu tu, lakini sisi tuna Yawe, Mungu wetu, kwa kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Maneno haya ya mufalme Hezekia yakawatia moyo sana watu wale.


Mimi nitawaimarisha watu wangu, nao watanitii na kuishi kwa kunipendeza. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Musiogope maana mimi nipo pamoja nanyi. Nitawarudisha wazao wenu toka mashariki, nitawakusanya ninyi kutoka magaribi.


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Yawe anasema hivi: Wakati uliofaa nilijibu maombi yako; wakati wa wokovu nilikusaidia. Nimekuweka na kukufanya ukuwe kiungo cha agano langu na mataifa yote: utatengeneza inchi na kurudisha tena inchi hiyo iliyoharibika.


Maana nguvu za waovu zitavunjwa, lakini Yawe atawaimarisha watu wa haki.


Mimi, Yawe Muumba wako, niliyekutengeza tangia tumbo la mama yako, ninakuja kukusaidia wewe. Mimi Yawe ninasema hivi: Musiogope, enyi wazao wa Yakobo, mutumishi wangu, usiogope, ewe Yeshuruni, muchaguliwa wangu.


Uniokoe kutoka upanga wa waadui wakali, uniokoe kutoka makucha ya wageni, ambao wanasema maneno ya uongo, wanaonyoosha mukono kwa kushuhudia uongo.


Hivyo nitajua kwamba unapendezwa nami, waadui zangu wasipopata ushindi juu yangu.


Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika; Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.


Ni furaha kabisa! Mujumbe anatokea kwenye mulima. Anatangaza habari njema za amani, heri, na ukombozi. Anauambia Sayuni: Mungu wako anatawala!


Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Heri wale unaowachagua na kuwaleta karibu, waishi katika kiwanja chako. Sisi tutatoshelewa na mazuri ya nyumba yako, mazuri ya hekalu lako takatifu.


Halafu malaika akamwambia: “Maria, usiogope, kwa maana Mungu amekujalia neema.


Umusifu Yawe, ee Yerusalema! Umusifu Mungu wako, ee Sayuni!


Daudi akatoka inje kwa kuwapokea, akawaambia: “Ikiwa mumekuja kwangu kama warafiki kwa kunisaidia basi ninawapokea kwa moyo wote, lakini kama mumekuja kwa kunitoa kwa waadui zangu, ingawa sijatenda ovu lolote, Mungu wa babu zetu awaone na kuwaazibu ninyi.”


Lakini yule malaika akamwambia: “Zakaria, usiogope, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Muke wako Elizabeti atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yoane.


Ee mufalme mukubwa, mupenda haki, umesimamisha usawa katika Israeli; umeleta sheria na haki.


ambao wanasema maneno ya uongo na kunyoosha mukono kwa kushuhudia uongo.


Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Si wangu”, maana ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.


Yakobo akawaambia: “Unaona kwamba baba yenu hanijali tena kama vile mbele. Lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami.


Lakini upinde wake bado imara, na mikono yake imepewa nguvu, kwa uwezo wa Mwenye Nguvu wa Yakobo, kwa jina la Muchungaji, Mulinzi wa Israeli.


Musa akawaambia Waisraeli: “Musiogope! Musimame imara! Leo mutaona jinsi Yawe atakavyowaokoa. Maana, hawa Wamisri munaowaona leo, hamutawaona tena.


Musa akawaambia: Musiogope, maana Mungu amekuja kuwapima kusudi mupate kumwogopa siku zote na musitende zambi.


Angalia Bwana wetu Yawe ananisaidia. Ni nani anayeweza kusema niko na kosa? Waadui zangu wote watachakaa kama nguo, nondo watawatafuna.


Wale watu kwa pamoja wakamwendea mufalme Dario na kumwambia: Ee mufalme, ujue kwamba hakuna sheria wala amri yoyote ya Wamedi na Wapersi inayoweza kubadilishwa kisha kuwekwa na mufalme.


Kwa hiyo yeye akaniambia: Danieli, usiogope. Mungu alisikia maombi yako tangu siku ile ya kwanza ulipoamua kujinyenyekeza mbele yake kusudi upate ufahamu. Mimi nimekuja kwa ajili ya maombi yako hayo.


Kisha Hagai, mujumbe wa Yawe, akawapa watu ujumbe huu kutoka kwa Yawe: Mimi niko pamoja nanyi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mulipotoka Misri niliwaahidi kwamba nitakuwa pamoja nanyi siku zote. Basi, ningali pamoja nanyi, kwa hiyo, musiogope kitu.


Usiku uleule Yawe alimutokea na kumwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako Abrahamu. Usiogope; niko pamoja nawe. Nitakubariki na kuwazidisha wazao wako kwa ajili ya Abrahamu, mutumishi wangu.”


Yawe akamwambia: “Nitakuwa pamoja nawe; nawe utawaangamiza Wamidiani sawa vile wangekuwa mutu mumoja.”


Walinishambulia nilipokuwa katika taabu, lakini Yawe alinikinga.


Umenipa ngao yako ya wokovu na kuniimarisha kwa mukono wako wa kuume. Nimefanikiwa kwa sababu ulikubali kunisaidia.


Heri taifa ambalo Mungu wake ni Yawe; heri wale aliowachagua kuwa watu wake mwenyewe!


Muwaambie waliovunjika moyo: Mujipe moyo, musiogope! Muangalie Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi, atakuja kuwaazibu waadui zenu; atakuja yeye mwenyewe kuwaokoa ninyi.


aliwaambia: “Mumwambie bwana wenu kwamba Yawe anasema hivi: Usiogope kwa sababu ya maneno uliyoyasikia, ambayo watumishi wa mufalme wa Asuria wameyasema kwa kunitusi.


Nilipokuita ulifika karibu nami ukaniambia: Usiogope!


Nitawaimarisha watu wa Yuda; nitawaokoa wazao wa Yosefu. Nitawarudisha kwao kwa maana ninawaonea huruma, nao watakuwa kama vile sikuwa nimewakataa. Mimi ni Yawe, Mungu wao, nami nitayasikiliza maombi yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite