Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 40:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kisha utukufu wa Yawe utafunuliwa, na watu wote pamoja watauona. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.

Gade chapit la Kopi




Isaya 40:5
39 Referans Kwoze  

Utukufu wa Yawe utaenea pote katika dunia, kama vile maji yanavyoenea katika bahari.


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Kila mutu ataona jinsi Mungu atakavyotuokoa.’ ”


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Simama, ee Sayuni uangaze; maana mwangaza unatokea kwa ajili yako, utukufu wa Yawe unakuangazia.


Katika mulima mutakatifu wa Mungu hakutakuwa ubaya wala uharibifu. Maana kumujua Yawe kutaenea pote katika inchi, kama vile maji yanavyojaa katika bahari.


utapata furaha yako kwangu mimi Yawe, nitakupatia ushindi katika kila upinzani katika inchi, nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Walilalamikiana mumoja kwa mwengine hivi: Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yawe wa majeshi! Dunia yote imejaa utukufu wake.


Jina lake tukufu litukuzwe milele; utukufu wake ujae katika ulimwengu wote! Amina, Amina!


Muji ule hauna lazima ya mwangaza wa jua, wala wa mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu unauangazia na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.


‘Mungu anasema: Katika siku za mwisho, nitashusha Roho wangu juu ya watu wote; wana wenu na wabinti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono nao wazee wenu wataota ndoto.


Katika kila sikukuu ya mwandamo wa mwezi, na katika kila siku ya Sabato, wanadamu wote watakuja kuniabudu. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.


Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliona kwa mbali utukufu wa Yesu, naye alisema habari zake.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.


Lakini mukikataa na kuniasi, mutaangamizwa kwa upanga. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Kila mutu atakaa kwa amani chini ya miti ya tini na mizabibu yake, bila kutishwa na mutu yeyote. –Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe wa majeshi.


Yawe akajibu na kusema hivi: Ni kwa sababu wamekataa kushika sheria yangu niliyowapa, wamekataa kutii sauti yangu na kufuata mapenzi yangu.


Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.


Litachanua maua kwa wingi kama waridi, litashangilia na kuimba kwa furaha. Mungu atalijalia utukufu wa milima ya Lebanoni, uzuri wa mulima Karmeli na wa bonde la Saroni. Watu watauona utukufu wa Yawe, watauona ukubwa wa Mungu wetu.


Mataifa yataheshimu jina la Yawe; wafalme wote katika dunia wataogopa utukufu wake.


Heshima na sifa vinamuzunguka; nguvu na uzuri vinajaza hekalu lake.


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Mimi ni Yawe, Mungu wa watu wote. Hakuna lolote linaloweza kunishinda.


Yawe atatoa hukumu kwa moto atawaazibu watu wote kwa upanga; nao atakaowaangamiza watakuwa wengi.


Tena, kesho asubui mutaona utukufu wa Yawe maana ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie?”


Mbingu zinatangaza haki yake; na mataifa yote yanauona utukufu wake.


Musome katika kitabu cha Yawe: Hakuna hata kiumbe kimoja kitakachokosekana, kila kimoja kitakuwa na mwenzake. Maana kinywa cha Yawe kimeamuru hivyo. Roho yake itawakusanya hao wote.


Kila bonde litafunikwa, kila mulima na kilima vitasawanishwa; njia zenye lukumba zitanyooshwa, nazo zenye mashimo zitalainishwa.


Watu wataona jambo hilo, nao watatambua na kuelewa kwamba mimi Yawe nimetenda hayo, mimi Mutakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.


Mutu yeyote wa jamaa ya Yeroboamu atakayekufia katika muji, imbwa watamukula; na yeyote atakayekufia katika shamba, ndege watamukula.’ Yawe amesema hivyo.”


Yawe atajenga upya Sayuni, na kuonyesha utukufu wake.


Umezidisha taifa letu, ee Yawe, umelizidisha taifa letu. Umeipanua mipaka yote ya inchi, kwa hiyo wewe unatukuzwa.


Ninayajua matendo yao na mawazo yao. Ninakuja kuwakusanya watu wa mataifa yote na wa luga zote, wakusanyike pamoja na kuuona utukufu wangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite