Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 38:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: Yawe anasema hivi: Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.

Gade chapit la Kopi




Isaya 38:1
16 Referans Kwoze  

Wakati ule, Hezekia akagonjwa sana, karibu kufa. Akamwomba Yawe, naye akamujibu na kumwonyesha kitambulisho.


Ahitofeli alipoona kwamba shauri lake halikufuatwa, alitandika punda wake, akaenda kwake, kwenye muji wake. Alipofika kule, alipanga vizuri mambo ya nyumba yake, akajitundika. Akakufa na kuzikwa kwenye kaburi la baba yake.


Mungu alipoona walivyofanya, na jinsi walivyouacha uovu wao, akabadilisha nia yake, akaacha kuwatenda kama alivyokuwa amekusudia.


Katika siku zile akapata ugonjwa, naye akakufa. Walipokwisha kunawisha maiti yake, wakailalisha ndani ya chumba cha gorofi.


Alipofika, Yona aliingia katika muji. Kisha kutembea mwendo wa siku nzima, akaanza kutangaza: Kunabaki siku makumi ine tu na muji huu wa Ninawe utaangamizwa!


Kisha Isaya mwana wa Amozi alituma ujumbe kwa Hezekia, akisema: Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwa sababu umeniomba juu ya Saniharibu mufalme wa Asuria,


Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, katibu, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.


Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


Daudi akawajibu: “Ni kweli mutoto alipokuwa muzima, nilifunga na kulia. Nilifanya hivyo maana nilifikiri: ‘Nani anajua? Labda Yawe atanihurumia kusudi mutoto aishi’.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite