Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 37:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Nao wakamwambia Isaya: “Hezekia anasema hivi: Leo ni siku ya huzuni, ya kuazibiwa, na ya kuzarauliwa. Sisi tumekuwa kama mwanamuke anayetaka kuzaa mutoto, lakini hana nguvu ya kumuzaa.

Gade chapit la Kopi




Isaya 37:3
20 Referans Kwoze  

Maumivu kama ya kuzaa mutoto yanamufikia. Lakini yeye ni mutoto mupumbafu; wakati wa kuzaliwa unapofika yeye anakataa kutoka ndani ya tumbo la mama!


Namna gani ninaweza kumufikisha mutoto kwa saa ya kuzaliwa, halafu nimuzuize asizaliwe? –Ni Yawe anayesema hivyo.– Au mimi mwenye kuwajalia watoto, namna gani nitafunga uzazi? –Ni Mungu wenu anayesema hivyo.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Nao wakamwambia Isaya: “Hezekia anasema hivi: ‘Leo ni siku ya huzuni, ya kuazibiwa na ya kuzarauliwa. Sisi tumekuwa kama mwanamuke anayetaka kuzaa mutoto, lakini hana nguvu ya kumuzaa.


Ee Yawe, utuonee huruma, kwako tumeliweka tumaini letu. Ukuwe kikingio chetu kila siku, mwokozi wetu wakati wa taabu.


“Musikuwe wagumu kama kule Meriba, kama ilivyokuwa kule Masa katika jangwa,


Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.


Lakini walipopatwa na shida, walimugeukia Yawe, Mungu wa Israeli, wakamutafuta, wakamupata.


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


Maana leo Yawe wa majeshi ametuletea fujo, kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono. Kuta za muji zimebomolewa. Kilio cha wakaaji wake kinasikilika mpaka kwenye milima.


Nitarudi mahali pangu na kujitenga nao mpaka watambue kosa lao na kunirudilia. Taabu zao zitawafundisha wanitafute.


Kweli, siku hiyo ni kubwa, hakuna ingine kama hiyo; ni siku ya taabu kwa watu wa Yakobo; hata hivyo, wataokolewa toka humo.


Bwana wetu Yawe atakiangamiza kifo milele! Atayafuta machozi katika nyuso za watu wote na kuondoa haya ya watu wake katika dunia yote. Yawe amesema hivyo.


Ee Yawe, walipotaabika walikutafuta, walikuomba musaada ulipowaazibu.


Muji wangu mutakatifu, ni kama mama anayezaa bila kupata uchungu; mbele ya uchungu kuanza, amekwisha zaa mutoto.


Siku nitakapotoa azabu, Efuraimu itakuwa kama jangwa! Ninachotangaza kati ya makabila ya Israeli, ni jambo litakalotukia kwa hakika.


lakini mimi Mungu nitahuzunisha Yerusalema, ndani yake kutakuwa vilio na maombolezo, muji wenyewe utakuwa kama mazabahu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite