Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 34:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Maiti zao zitatupwa inje; harufu ya maiti zao itasambaa; damu yao itatiririka juu ya milima.

Gade chapit la Kopi




Isaya 34:3
20 Referans Kwoze  

Nitawaondoa hao waadui wanaotoka kaskazini, nitawafukuza mpaka katika jangwa; waaskari wa mbele nitawatupa katika bahari ya Chumvi na wale wa nyuma katika bahari ya Mediteranea. Watatoa uvundo na harufu mbaya, hao ambao wamefanya maovu makubwa.


Utakufa juu ya milima ya Israeli, wewe pamoja na makundi yako yote ya waaskari na mataifa yanayokuwa pamoja nawe. Nami nitaitoa miili yao ikuliwe na ndege wa kila aina na nyama wakali.


Mbogo wataangamizwa pamoja nao, wana-ngombe pamoja na ngombe dume. Inchi italewa na damu, udongo utashiba kwa mafuta yao.


Zile zabibu zikakamuliwa mbali na muji, damu ikatiririka toka ndani ya kile kikamulio mpaka ikafika kwenye umbali wa kilometre yapata mia tatu. Nao urefu kwenda chini wa ile damu ulikuwa yapata metre moja na nusu.


Niliwaletea ugonjwa mukali kama ule nilioupelekea Misri. Niliwaua vijana wenu katika vita, nikatwaa farasi wenu wa vita. Maiti zilijaa katika kambi zenu, harufu yake mbaya ikajaa katika pua zenu. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Katika siku ile, nitamupa Gogi pahali pa kufanyia maziko katika inchi ya Israeli, katika Bonde la Wasafiri, upande wa mashariki wa bahari ya Chumvi. Gogi atazikwa huko pamoja na kundi lake lote la waaskari, nao wasafiri watazuizwa kupita kule. Bonde hilo litaitwa, Bonde la Hamoni-Gogi.


Nitamwazibu Gogi kwa ugonjwa mukali na mauaji. Nitanyesha mvua nyingi na mvua ya mawe na moto na kiberiti juu yake, juu ya makundi yake, na mataifa yale mengi yanayokuwa pamoja naye.


Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– kifo kinakungoja na hautaweza kukiepuka. Uko na makosa ya mauaji, basi mauaji nayo yatakuandama.


Tena nitaleta ugonjwa mukali katika inchi ile na kwa kasirani yangu nitawaua watu na nyama.


Yeye atazikwa sawa nyama: atakokotwa na kutupiliwa mbali, inje ya milango ya Yerusalema.


Hakuna! Mutajikunja tu kati ya wafungwa na kuangamia pamoja na wanaouawa katika vita. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Kisha watakwenda kuziona maiti za wale walioniasi. Wadudu watakaowakula hawatakufa, na moto utakaowachoma hautazimika hata kidogo. Watakuwa chukizo kwa watu wote.


Siku hiyo, wale watakaouawa na Yawe watasambaa kutoka upande mumoja wa dunia mpaka upande mwingine. Hakuna atakayeomboleza juu yao, wala maiti zao hazitakusanywa wala kuzikwa; zitabaki sawa mboleo juu ya udongo.


Waaskari wapanda-farasi wanashambulia, panga na mikuki inametameta; waliouawa hawana hesabu, kuna maiti nyingi sana; watu wanajikwaa juu ya maiti!


Nitakutupa juu ya inchi kavu, nitakutupa chini juu ya uwanja, nitaleta ndege wote watue juu yako, na kuwashibisha nyama wote wa pori kwa mwili wako.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite