Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 33:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Ee Yawe, utuonee huruma, kwako tumeliweka tumaini letu. Ukuwe kikingio chetu kila siku, mwokozi wetu wakati wa taabu.

Gade chapit la Kopi




Isaya 33:2
35 Referans Kwoze  

Aliona kwamba hakuna mutu aliyejali, akashangaa kwamba hakuna aliyeingilia kati. Basi akaamua kunyoosha mukono wake mwenyewe, haki yake ikamusaidia.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Ni nani atakayenipeleka kwenye muji unaozungukwa na kuta? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?


Wokovu na utukufu wangu vinatoka kwa Mungu; kikingio changu chenye nguvu na kimbilio langu ni Mungu.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora: Kwa mutindo wa Sauti ya juu kabisa.


Basi, Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari na kulipopambazuka bahari ikarudilia hali yake ilivyokuwa. Wamisri wakajaribu kukimbia maji lakini Yawe akawasukumizia ndani ya bahari.


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Uaminifu wake ni mukubwa sana, kila mara kunapokucha ni mupya kabisa.


Wewe unayekuwa tumaini la Waisraeli, wewe unayetuokoa wakati wa taabu, namna gani unajifanya kama mugeni katika inchi, kama musafiri anayelala kwa usiku mumoja tu?


Bwana wetu Yawe anakuja na nguvu, kwa mukono wake anatawala. Yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Ee Yawe, walipotaabika walikutafuta, walikuomba musaada ulipowaazibu.


Katika njia ya maamuzi yako tunakungojea ee Yawe; tamaa yetu ni kulikumbuka jina lako.


Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;


Kama watumishi wanavyomutegemea bwana wao, kama mujakazi anavyomutegemea bibi mukubwa wake, ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe, ee Yawe, Mungu wetu, mpaka hapo utakapotuonea huruma.


Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.


Utujalie sasa miaka mingi ya furaha, kama ulivyotupa miaka mingi ya shida na taabu.


Mumepanga kuniangusha toka nafasi yangu ya heshima; furaha yenu ni kusema uongo. Kwa maneno, munabariki, lakini ndani ya moyo munalaani.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Kuna muto ambao maji yake yanafurahisha muji wa Mungu, makao matakatifu ya Mungu Mukubwa.


Yawe anawaokoa watu wa haki, na kuwalinda wakati wa taabu.


Usimwache anayekutumainia kupata haya; lakini wafezeheke wote wanaokuasi kwa makusudi.


Kila asubui unionyeshe wema wako, maana ninakutumainia. Unifundishe mwenendo wa kufuata, maana ninakutolea moyo wangu.


Zaburi ya Daudi. Yawe ni mwangaza wangu na wokovu wangu, ni nani nitakayemwogopa? Yawe ni mulinzi wa maisha yangu, sitamwogopa mutu yeyote.


Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;


Nao wakamwambia Isaya: “Hezekia anasema hivi: Leo ni siku ya huzuni, ya kuazibiwa, na ya kuzarauliwa. Sisi tumekuwa kama mwanamuke anayetaka kuzaa mutoto, lakini hana nguvu ya kumuzaa.


Ukombozi wangu unakaribia upesi; wokovu nitakaoleta unaanza kutokea. Mimi mwenyewe nitayatawala mataifa. Wakaaji wa inchi za mbali wananingojea, wanaitegemea nguvu yangu.


Wema wako ukae nasi, ee Yawe, kwa maana tumekuwekea tumaini letu.


Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite