Yawe anasema: Wanawake wa Sayuni wako na kiburi; wanatembea wakiinua kichwa juu, wakirembua macho yao kwa tamaa. Hatua zao ni za maringo, nao wanalilisha mikufu kwenye miguu yao.
Basi huu ndio muji uliojivuna na kuishi kwa usalama, muji uliojisemesha: Ni mimi tu, hakuna mwingine! Jinsi gani umekuwa mutupu na makao ya nyama wa pori! Kila mutu anayepita karibu atauzomea na kuuzarau.
Yotamu alipopata habari hiyo, alikwenda kusimama juu ya mulima Gerizimu, akasema kwa sauti kubwa: “Munisikilize, enyi watu wa Sekemu kama munataka Mungu awasikilize.
Hata mwanamuke yule ambaye ni mupole sana na aliyelelewa vizuri na mwenye kupendeza ambaye hajasubutu kukanyaga udongo kwa kikanyagio chake, hatafurahi kuona mume wake aliyemupenda na watoto wake. Wakati huo wa kuzungukwa kutakuwa njaa hata
Kifo kimetuingilia katika madirisha yetu, kimetupangia katika nyumba zetu nzuri; kimewaangukia watoto wetu katika barabara, nao vijana wetu katika viwanja vya makutano.
Enyi wanawake, musikilize neno la Yawe! Mutege masikio musikie jambo analosema. Muwafundishe wabinti zenu kuomboleza, na kila mutu amufundishe jirani yake wimbo huu wa maziko: