Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 32:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Macho ya wanaoona hayatapofushwa tena, masikio ya wanaosikia yatabaki wazi.

Gade chapit la Kopi




Isaya 32:3
14 Referans Kwoze  

Siku hiyo viziwi watasikia ujumbe ukisomwa katika kitabu na kutoka katika giza, vipofu wataanza kuona.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Nao watu wakashangaa sana na kusema: “Mambo anayofanya ni mazuri kweli. Anawawezesha hata viziwi wasikie, nao wabubu wapate kusema.”


Watu wako watafundishwa nami Yawe, wana wako watapata ustawi mwingi.


Waliopotoka katika roho watapata maarifa na wenye kunungunika watakubali kufundishwa.


Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa mbinguni, lakini kwao si vile.


Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.


Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.


Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao nitaligeuza giza kuwa mwangaza, na pahali penye kuharibika patakuwa laini. Huo ndio mupango wangu wa kufanya, nami nitautimiza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite