Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 32:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Katika mwaka mumoja hivi mutatetemeka ninyi muliotosheka; maana hamutapata mavuno yoyote, na mavuno ya mizabibu yatatoweka.

Gade chapit la Kopi




Isaya 32:10
14 Referans Kwoze  

Nilitaka kuchuma matunda kutoka kwao. –Ni ujumbe wa Yawe.– Lakini sikupata zabibu hata moja juu ya muzabibu, sikupata tini zozote juu ya muti wa tini; hata majani yao yamekauka. Hata nilichokuwa nimewapa kimetoweka.


Wakati huo, kila pahali palipokuwa mizabibu elfu moja iliyopata vikoroti vya feza elfu moja, patakuwa michongoma na miiba mitupu.


Utajiri wao utanyanganywa, na nyumba zao zitaachwa tupu! Watajijengea nyumba, lakini hawataishi humo. Watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.


Hata kama miti ya tini isipochanua maua wala mizabibu kuzaa zabibu, hata kama mizeituni isipozaa zeituni na mashamba yasipotoa chakula, hata kama kondoo wakitoweka katika zizi na nyama wa kufugwa kukosekana katika mazizi,


Mizabibu imenyauka, mitini imekauka, miti yote ya matunda imekauka. Furaha imetoweka kati ya watu.


Limeiharibu mizabibu yetu, na kuitafuna mitini yetu. Limeyabandua maganda yake na kuyatupa chini, na matawi yake yameachwa meupe.


Hivi ndivyo Waisraeli watakavyokuwa: watakaa kwa muda murefu bila mufalme au mukubwa; bila sadaka, wala nguzo za sanamu wala vyombo walivyotumia kwa kujua mapenzi ya Mungu.


Nitamuvua nguo abaki uchi mbele ya wapenzi wake, wala hakuna mutu atakayeweza kunizuia.


Furaha na shangwe zimetoweka katika shamba lenyi mavuno mengi. Kwenye mizabibu hakuna kuimba tena, wala kupiga vigelegele. Hakuna tena kukamua zabibu ndani ya vikamulio, sauti za furaha za mavuno zimekomeshwa.


Enyi walevi, muamuke na kulia; enyi walevi wa divai, mulalamike; zabibu zote za kutengeneza divai mupya zimeharibiwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite