Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 30:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ole watoto waasi, wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu! –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.

Gade chapit la Kopi




Isaya 30:1
48 Referans Kwoze  

Muchana kutwa niliwanyooshea mikono watu waasi, watu ambao wanafuata njia zisizokuwa nzuri, watu ambao wanafuata mawazo yao wenyewe.


Yawe anasema hivi: Sikiliza enyi mbingu, tega sikio ee dunia. Mimi nimewalea watoto wangu na kuwakomalisha, lakini sasa wameniasi!


Ole kwao kwa sababu wameniacha! Maangamizi yawapate, maana wameniasi. Nilitaka kuwakomboa, lakini wanasema uongo juu yangu.


Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.


Lakini wao waliasi, wakaihuzunisha roho yake takatifu. Basi, Mungu akageuka, akakuwa adui yao; yeye mwenyewe akapigana nao.


Ole kwenu ninyi munaomuficha Yawe mipango yenu, munaotenda matendo yenu katika giza na kusema: Hakuna atakayetuona; nani anayeweza kujua tunachofanya?


Lakini watu waovu na wadanganyifu wataendelea katika maovu, wakipotosha watu wengine na kujipotosha wenyewe.


Kama vile almasi inavyokuwa ngumu kuliko mawe mengine, ndivyo nilivyokufanya ukuwe na kichwa kigumu. Usiwaogope wala usitishwe na nyuso zao, maana hao ni watu waasi.


akiniambia hivi: Wewe mwanadamu ninakutuma kwa Waisraeli, taifa la waasi ambao wameniasi. Wameendelea kunikosea mimi mpaka leo sawa vile babu zao walivyofanya.


Lakini watu hawa wana moyo mugumu na wa uasi; wamegeuka na kuniacha.


Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminiwa; watu wasiopenda kusikia mafundisho ya Yawe.


Wewe ndiwe kimbilio langu, boma langu lenye nguvu la kukimbilia waadui.


Yawe hatasamehe mutu huyo, nayo hasira ya Yawe na wivu wake vitamuwakia mutu huyo. Laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki zitamupata, naye Yawe atafuta kabisa jina la mutu huyo kutoka katika dunia.


Ninyi mumekuwa waasi mbele ya Yawe tangu siku nilipowajua.


wanauzunguka Yerusalema kama walinzi wanavyozunguka mashamba, kwa sababu watu wake wameniasi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.


Musijiunge nao katika mashauri yao mabaya, wala musiogope yale wanayoyaogopa wala kuwa na hofu.


Halafu, kila pahali juu ya mulima Sayuni na juu ya mikutano ya watu atafanya kuwe wingu wakati wa muchana, na moshi na moto unaowaka vizuri wakati wa usiku. Zaidi ya hayo utukufu wa Mungu utaufunika na kuulinda muji wote.


Niwapige wapi tena, ninyi munaoendelea kuasi? Kichwa chote kinajaa vidonda, na moyo unaumia kabisa!


Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!


Ole kwao wanaokokota uovu kama kwa kamba; wanaoburura zambi kama wanavyokokota gari.


Kwenu itakuwa kama anayejinyoosha juu ya kitanda kifupi sana, au kujifunika kwa blanketi inayokuwa ndogo sana!


Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!


Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima.


“Mukumbuke na musisahau jinsi mulivyomukasirikisha Yawe, Mungu wenu, kule katika jangwa. Tangu siku ile mulipotoka katika inchi ya Misri mpaka siku mulipofika pahali hapa, ninyi mumekuwa mukimwasi Yawe.


Na sasa, enyi kizazi cha wenye zambi, mumesimama kwa pahali pa wazee wenu, kuongeza tena hasira kali ya Yawe juu ya Waisraeli.


Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Yawe alinionya kwa nguvu nisifuate njia za watu hawa, akaniambia:


Yawe anasema hivi: Alaaniwe mutu anayemutegemea mwanadamu, mutu ambaye anategemea nguvu za mwanadamu, mutu ambaye moyo wake umegeuka mbali nami Yawe.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Utamwambia mufalme wa Yuda hivi ambaye amekutuma uniombe kwa ajili yake: Waaskari wa Mufalme wa Misri waliokuja kukusaidia, wako karibu kurudia kwao Misri.


Yeremia akawaambia watu: Enyi Wayuda muliobaki, Yawe aliwaambia musiende Misri. Mujue wazi kwamba leo nimewaonya kwamba


Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu, hawa ndio watu wanaofanya mipango ya uovu na kutoa mashauri mabaya katika muji huu.


Uwape mufano hao watu wangu waasi na kuwaambia kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Weka chungu juu ya mafika, ukijaze maji vilevile.


Misri haitakuwa tena na nguvu za kuweza kutegemewa na Waisraeli. Waisraeli watakumbuka jinsi walivyokosa kwa kutegemea inchi ya Misri. Waisraeli watatambua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.


Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.


Hivyo, Waisraeli wakatwaa vyakula vyao, bila kumwuliza Yawe shauri.


Angalia sasa. Unategemea Misri, utete uliovunjika ambao utamuchoma mukono mutu yeyote atakayeutegemea. Hivi ndivyo mufalme wa Misri anavyokuwa kwa wote wale wanaomutegemea.


Hata kama munategemea Misri kupata magari ya vita na waaskari wapanda-farasi, hamuwezi kumurudisha nyuma mutu mumoja wa cheo cha chini sana kati ya watumishi wa bwana wangu.


Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Na sasa itakufalia nini kwenda Misri kunywa maji ya muto Nili? Au itakufalia nini kwenda Asuria kunywa maji ya muto Furati?


Upanga utavuma katika miji yao, utavunjavunja miimo ya milango yake na kuwaangamiza katika kuta zao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite