Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.

Gade chapit la Kopi




Isaya 3:9
30 Referans Kwoze  

Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda zambi wakubwa mbele ya Yawe.


Wao walisikia haya walipofanya machukizo hayo? Hapana! Hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo wataanguka pamoja na wale wanaoanguka; wakati nitakapowaazibu, wataangamizwa kabisa. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Kwa maana mushahara wa zambi ni kifo, lakini zawadi Mungu anayotoa ni uzima wa milele kwa kuungana na Yesu Kristo, Bwana wetu.


Alipoziona picha hizo, mara moja akashikwa na tamaa, akatuma wajumbe kwenda Kaldea.


Taji tuliojivunia imeanguka. Ole kwetu maana tumetenda zambi!


Ndiyo maana manyunyu yamezuizwa kuanguka, wala mvua za mwisho hazijanyesha. Hata hivyo unakausha macho kama kahaba, wala hauna haya hata kidogo.


Yawe anasema: Wanawake wa Sayuni wako na kiburi; wanatembea wakiinua kichwa juu, wakirembua macho yao kwa tamaa. Hatua zao ni za maringo, nao wanalilisha mikufu kwenye miguu yao.


Kuna watu ambao macho yao yanajaa kiburi. Wanazarau kila kitu wanachoona.


Asiyenipata anajizuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”


Katika majivuno yake anasema: “Mungu hatagundua. Hakuna Mungu.” Hayo ndiyo mawazo yake yote.


Yehu alipofika Yezereheli, Yezebeli alikuwa amekwisha kupata habari ya mambo yaliyotokea. Alijipakaa rangi kwenye macho na kuchanua nywele zake, kisha akaenda kwenye dirisha na kuangalia chini.


Kisha Samweli akasema: “Muniletee hapa Agagi mufalme wa Waamaleki.” Agagi akamwendea Samweli akiwa mwenye furaha maana alifikiri: “Uchungu wa kifo umepita.”


Nitawaangamiza, enyi Waisraeli. Nani ataweza kuwasaidia?


Vilevile nilitaka nielezwe juu ya zile pembe kumi alizokuwa nazo juu ya kichwa chake, na ile pembe moja iliyoota na pembe zingine tatu zilizoanguka mbele yake, ndiyo ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa ambacho kilisema maneno ya kujivuna, na ambayo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine.


Maiti zao zitabaki katika barabara ya muji ule mukubwa unaoitwa kwa fumbo Sodoma au Misri. Ni ndani ya muji ule Bwana wao alitundikwa juu ya musalaba.


lakini hakupendezwa na Kaina wala na sadaka yake. Basi, Kaina akakasirika sana na uso wake ukakunjamana.


Anayekataa kufundishwa anajizarau mwenyewe, lakini anayekubali maonyo anapata ufahamu.


Musikilize neno la Yawe, enyi watawala waovu kama wa Sodoma! Musikilize mafundisho ya Mungu wetu, enyi watu waovu kama wa Gomora!


Lakini waovu ni kama bahari iliyochafuka, ambayo haiwezi kutulia; maji yake yanatupa matope na takataka.


Makosa yetu mbele yako ni mengi sana, zambi zetu zinashuhudia juu yetu. Kweli, makosa yetu yanaandamana nasi, tunayajua maovu yetu.


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Walisikia haya walipotenda machukizo hayo? Hapana, hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka; nitakapowaazibu, wataangamia. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Kweli wewe ni mugonjwa wa mapenzi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Unafanya uzinzi bila kuona haya hata kidogo.


Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.


Kesho yake, yule binti wa kwanza akamwambia yule mudogo: “Jana usiku mimi nililala na baba. Leo vilevile tumuleweshe kwa divai, kisha wewe utalala naye, na hivyo sisi wote tutadumisha uzao kwa kupata watoto.”


Kiburi cha Waisraeli kinaonekana wazi; watu wa Efuraimu watajikwaa katika makosa yao, nao watu wa Yuda watajikwaa pamoja nao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite