Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 3:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 pete za masikio, vikomo na vitambaa vya ushungi,

Gade chapit la Kopi




Isaya 3:19
14 Referans Kwoze  

Nikakupamba kwa mapambo, nikakuvalisha vikomo kwa mikono yako na mukufu kwenye shingo.


Basi, tumeleta vyombo vya zahabu, mikufu, vikomo, pete za muhuri, pete za masikio na ushanga ambavyo kila mutu alipata. Tumevitoa kusudi nafsi zetu zifanyiwe upatanisho mbele ya Yawe.


Hivyo wote wenye moyo safi, wanaume na wanawake, wakaleta pete za masikio na za muhuri, vikuku na kila aina ya mapambo ya zahabu. Kila mutu akamutolea Yawe kitu cha zahabu.


Yuda akamwuliza: “Unataka nikupe nini kama rehani?” Naye akamujibu: “Unipe hiyo pete na kamba yake pamoja na hiyo fimbo unayoshika.” Basi, Yuda akamupa vitu hivyo vyote, akalala naye. Tamari akapata mimba yake.


Kisha akatoa vyombo vya feza na zahabu na nguo, akamupa Rebeka. Vilevile aliwapa wandugu na mama ya Rebeka mapambo ya bei kubwa.


Labani alikuwa ameona ile pete na vikomo kwa mikono ya dada yake na kusikia mambo Rebeka aliyoambiwa na yule mutu. Labani akamukuta yule mutu akisimama karibu na ngamia wake kando ya kisima.


Ngamia walipotosheka kunywa maji, yule mutu akamupa yule binti pete ya zahabu yenye uzito wa yapata grama sita, na vikomo viwili vya zahabu za grama kumi kila moja.


Walipokuwa wakimutoa inje, Tamari akatuma ujumbe kwa baba mukwe wake, akisema: “Mwenye vitu hivi ndiye aliyenipa mimba. Kwa hiyo, ninakuomba umutambue mwenye pete hii na kamba yake, na fimbo hii.”


Basi, wakamupa Yakobo sanamu zote za miungu ya kigeni walizokuwa nazo pamoja na pete walizokuwa wamevaa kwa masikio. Na Yakobo akavizika chini ya muti wa mwalo uliokuwa karibu na Sekemu.


Siku zinakuja ambapo Yawe atawanyanganya wanawake wa Yerusalema vitu vyote wanavyoringia: pete za miguu, vitana, mibano ya nywele,


vitambaa vya kichwa, mikufu, mikaba iliyosokotwa, hirizi na mikufu ya kuleta bahati,


Haruni akawajibu: Mutwae pete za zahabu za masikio ya wake zenu, wana wenu na wabinti zenu, muniletee.


Basi, watu wote wakatoa pete zote za zahabu za masikio yao, wakamuletea Haruni.


Nikakutia pete kwenye pua, visikio kwenye masikio yako na juu ya kichwa chako nikakupamba kwa taji nzuri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite