Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 28:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Bwana amejichagulia mutu wake shujaa na mwenye nguvu, ambaye ni kama mvua ya mawe na zoruba kali, kama zoruba ya mafuriko makubwa; kwa mukono wake atawatupa chini.

Gade chapit la Kopi




Isaya 28:2
21 Referans Kwoze  

Waadui wakishambulia inchi kama mafuriko, yeye anawaangamiza; anawafuatilia na kuwafukuza mpaka katika giza.


Sasa uwaambie hao manabii wanaopakaa chokaa ukuta huo kwamba kutanyesha mvua kubwa ya mawe na zoruba itavuma na ukuta huo utaanguka.


Yawe atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa ndimi za moto mukali, ngurumo, zoruba na mvua ya mawe.


Yawe wa majeshi atakuja kukusaidia; atakuja na ngurumo, tetemeko la inchi na sauti kubwa; atakuja na upepo mukali, zoruba na moto wenye kuunguza.


Siku hiyo, Yawe atakamata upanga wake mukubwa, mukali na imara, na kuiazibu Leviatani, ile nyoka inayoruka na kuzongazonga. Yawe ataua nyoka mukubwa anayeishi katika bahari.


Kwa sababu hiyo, kwa muda wa siku moja tu utapatwa na mapigo ya mauti, huzuni na njaa. Na zaidi ya hiyo utateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana wetu, Mungu anayeuhukumu, ni mwenye uwezo.”


Bwana wetu Yawe anakuja na nguvu, kwa mukono wake anatawala. Yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;


Malaika wa kwanza akapiga baragumu. Halafu mvua ya mawe na moto vyenye kuchanganyika na damu, vikatupwa katika dunia. Sehemu moja ya tatu ya inchi ikateketea, na sehemu moja ya tatu ya miti na majani yote vikateketea vilevile.


Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli kwenye muteremuko wa Beti-Horoni, Yawe akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka mbinguni wakiwa katika njia mpaka Azeka hata waliouawa kwa mawe hayo wakakuwa wengi kuliko waliouawa kwa silaha za Waisraeli.


Hao walifagiliwa mbele ya wakati wao, misingi yao imepelekwa mbali na maji.


Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Siloa yanayotiririka polepole, wakatetemeka mbele ya mufalme Resini na mufalme Peka mwana wa Remalia,


Pumzi yake ni kama mafuriko ya muto ambao maji yake yanafika mpaka kwenye shingo. Anakuja kupepeta mataifa kwa lungo ya maangamizi, kuwafunga lijamu na kuwapeleka wasikotaka.


Lakini mvua ya mawe itanyesha na kuangusha pori, na muji wake utaangamizwa.


Utakwenda mbio kama zoruba na kuifunika inchi kama wingu, wewe mwenyewe na kundi lako lote la waaskari pamoja na mataifa mengi yanayokuwa pamoja nawe.


Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite