Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 27:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Hivi ndivyo uovu wa wazao wa Yakobo utakavyoondolewa, hivi ndivyo zambi yake itakavyofutwa kabisa: ataziharibu mazabahu za miungu; mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa. Sanamu za Ashera wala mazabahu za kufukizia ubani hazitabaki.

Gade chapit la Kopi




Isaya 27:9
36 Referans Kwoze  

Na hili ndilo agano nitakalofanya nao, wakati nitakapowasamehe zambi zao.”


Mimi nimekusafisha lakini si kama feza katika furu. Nimewapima katika furu ya taabu.


Wamoja kati ya wenye hekima watauawa, kusudi wapate kuondolewa uchafu, kutakaswa na kusafishwa, mpaka wakati wa mwisho, ambao sasa bado haujatimia.


Hawataelekea tena mazabahu ambazo ni kazi za vidole vyao wenyewe, wala kuzitazamia tena kazi za mikono yao wenyewe, ni kusema sanamu za mungu Ashera na mazabahu za kufukizia ubani.


Kwa maana, Bwana anamwazibu yule anayemupenda, yeye anamupiga kila mutu anayemukubali kuwa mutu wake.”


Lakini tunahukumiwa na kuazibiwa na Bwana kusudi tusiazibiwe pamoja na watu wa dunia hii.


Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.


Watarudi na kuishi chini ya ulinzi wangu, watastawi kama bustani nzuri. Watachanua kama muzabibu, harufu yao nzuri kama ya divai ya Lebanoni.


Nitaondoa kati yenu waasi na wale wanaonikosea; nitawaondoa katika inchi walikokaa kama wakimbizi, lakini hawataingia hata kidogo katika inchi ya Waisraeli. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nanyi mutakaporudi katika inchi yenu nitaondoa vitu vyote vichafu na machukizo yote.


Bwana atawatakasa wanawake wa Sayuni toka uchafu wao na kusafisha damu iliyomwangika katika Yerusalema, kwa njia ya upepo wa hukumu na wa kuunguza.


Mutapata haya kwa ajili ya miti ya mialo muliyoipenda sana; mutafezeheka kwa sababu ya bustani mulizofurahia.


Mapigo yanayoumiza ni dawa ya kuondoa uovu; fimbo inasafisha nafsi mpaka ndani kabisa.


Nimefaidika kutokana na taabu yangu, maana imeniwezesha kujifunza masharti yako.


Mbele sijateswa nilikuwa nimepotea, lakini sasa ninashika neno lako.


Aliichoma moto nyumba ya Mungu, akaubomoa ukuta wa Yerusalema, akazichoma moto nyumba zote za kifalme na kuharibu vyombo vyake vyote vya bei kali.


Watu wake walibomoa mazabahu za ibada za Mabali mbele yake na alikatakata mazabahu za kufukizia ubani zilizoinuliwa juu ya mazabahu hizo; vilevile alipondaponda sanamu za Ashera na zingine za kuchonga na za kuyeyusha; akazifanya kuwa mavumbi, nayo mavumbi akayamwanga juu ya makaburi ya wale ambao walizitolea sadaka.


Alijenga miji yenye kuta za kuiimarisha inchi ya Yuda wakati ule wa amani, na kwa muda wa miaka ile, hapakutokea vita kwa maana Yawe alimupa amani.


Akaichoma kwa moto nyumba ya Yawe, nyumba ya kifalme na nyumba zote za Yerusalema; kila nyumba kubwa akaichoma kwa moto.


Lakini mutabomoa mazabahu zao na kuvunja nguzo zao za ibada na sanamu zao za Ashera.


Nitaharibu pahali penu pa ibada kule juu ya milima, nitabomoa mazabahu zenu za kufukizia ubani, na kutupa maiti zenu juu ya sanamu za miungu yenu. Roho yangu itawachukia kabisa.


Muvunje mazabahu zao, na kubomoa kabisa nguzo zao. Muteketeze kwa moto sanamu zao za Ashera na kukatakata sanamu zao za kuchonga na kufuta kabisa jina lao na pahali hapo.


na kutoa nguzo takatifu na kuiteketeza kwa moto.


Mazabahu zenu zitaharibiwa na pahali penu pa kufukizia ubani patavunjwavunjwa. Wale watakaouawa nitawatupa mbele ya sanamu zenu za miungu.


Alivunja nguzo vipandevipande; vilevile alikatakata sanamu za Ashera, na pahali zilipokuwa zinasimama akapajaza mifupa ya watu.


Mutazihesabu sanamu zenu za miungu zilizopakwa feza na zahabu kuwa uchafu. Mutazitupilia mbali kama takataka, mukisema: Mupotelee mbali!


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Nitakomesha matendo yenu ya uchawi, nanyi hamutakuwa tena na waaguzi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite