Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 26:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Maana Yawe anakuja kutoka kwake juu, kutoka makao yake huko mbinguni; kuwaazibu wakaaji wa dunia kwa uovu wao. Nayo dunia haitaficha tena wale waliouawa, lakini itaufichua umwagaji wa damu wote.

Gade chapit la Kopi




Isaya 26:21
28 Referans Kwoze  

Maana, Yawe ameniambia hivi: Tokea juu kwenye makao yangu nitaangalia yanayotukia, nikitulia kama joto katika mwangaza wa jua, kama wingu la umande wakati wa mavuno.


Yawe anasema hivi: Nitauazibu ulimwengu kwa uovu wake, waovu kwa sababu ya makosa yao. Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno, na kuporomosha mazarau ya watu wakali.


Ewe dunia, usifunike damu yangu iliyomwangika; kilio changu kienee kila pahali.


Watu hawa walimwanga damu ya watu wako na ya manabii wako, kwa sababu hiyo sasa umewakunywesha damu, nao wanastahili kutendewa vile!”


Basi watu wa kizazi hiki watabeba lazima ya damu ya manabii wote iliyomwangwa tangu kuumbwa kwa dunia,


Ninyi wapumbafu! Si Mungu aliyeumba inje ya mutu ndiye aliyeumba ndani yake vilevile?


Basi, Mungu akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, unaona mambo wanayofanya, machukizo makubwa Waisraeli wanayofanya kusudi wapate kunifukuza kutoka katika hekalu langu? Tena utaona machukizo mengine makubwa zaidi.


Muji Babeli umeazibiwa kwa sababu ndani yake kumeonekana damu ya manabii na ya watu wa Mungu pamoja na damu ya watu wote waliouawa katika dunia.


Mbingu zitafichua uovu wake, dunia itajitokeza kumushambulia.


Mutafanya nini siku ya azabu, siku zoruba itakapowakujia kutoka mbali? Mutamukimbilia nani kwa kuomba musaada? Mutakwenda wapi kwa kuweka mali yenu?


Yawe wa majeshi alinifunulia haya akisema: Hakika uovu huu hautasahauliwa mbele ya kufa kwenu. Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Yawe wa majeshi atakuja kukusaidia; atakuja na ngurumo, tetemeko la inchi na sauti kubwa; atakuja na upepo mukali, zoruba na moto wenye kuunguza.


Mujue kwamba mambo hayo yameandikwa mbele yangu, sitanyamaza lakini nitawalipiza; nitawalipa sawa inavyostahili.


Nitawalipiza maovu yao wayalipe vilevile maovu ya babu zao. –Ni Yawe anayesema hivyo.– Wao waliifukizia ubani miungu yao kwenye milima, wakanitukana mimi kule juu ya vilima. Nitawalipa sawa inavyostahili, watayalipa matendo yao ya zamani.


Musikilize: makelele kutoka katika muji, sauti kutoka katika hekalu! Hiyo ni sauti ya Yawe akiwaazibu waadui zake!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite